settings icon
share icon
Swali

Mkristo ana asili mbili?

Jibu


Tatizo la kwanza ambalo linakuja na swali hili ni moja ya elemu ya lugha ya maneno na jinsi yalivyo. Kwa mfano, wengi hupenda "asili ya dhambi," wengine wanapendelea "asili ya kuadhiriwa na dhambi," na wengine wanapendelea "mwili" usio na maana. Yoyote ni majina maalum ambayo hutumiwa kwa vyama vinavyopigana, jambo la muhimu ni kwamba vita vinavyoendelea vinaanzia miongoni mwa Wakristo.

Tatizo la pili ni ufafanuzi halisi wa "asili." Jinsi neno hili muhimu linalotafsiriwa huamua jinsi mtu anavyoona tofauti kati ya "mtu wa zamani" na "mtu mpya" na kazi yake inayofaa katika maisha ya Mkristo. Njia moja ya kutazama "asili" ni kuelewa kama "uwezo" ndani ya muumini. Kwa hiyo, mtu mzee anafafanuliwa kama njia ya zamani ya maisha, ya mtu asiyeamini. Kwa maana hii, Mkristo ana uwezo wa kupigana ndani yake-uwezo wa zamani wa dhambi na uwezo mpya wa kupinga dhambi. Asiyeamini hana ushindani kama huo ndani yake; hawana uwezo wa utauwa kwa sababu ana asili tu ya dhambi. Hiyo si kusema hawezi kufanya "matendo mema," lakini msukumo wake kwa kazi hizo daima unajisiwa na uovu wake. Kwa kuongezea, hawawezi kupinga dhambi kwa sababu hawana uwezo wa kuzuia dhambi.

Muumini, kwa upande mwingine, ana uwezo wa utauwa kwa sababu Roho wa Mungu anaishi ndani yake. Bado ana uwezo wa kutenda dhambi pia, lakini sasa ana uwezo wa kupinga dhambi na, muhimu zaidi, hamu ya kupinga na kuishi maisha ya kimungu. Wakati Kristo alisulubiwa, mtu wa kale alisulubiwa pamoja Naye, na kumfanya Mkristo asiwe tena mtumwa wa dhambi (Warumi 6: 6). "na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki" (Warumi 6:18).

Wakati wa kubadilika, Mkristo anapata asili mpya. Ni kitu hufanyika hapo hapo. Utakaso, kwa upande mwingine, ni mchakato ambao Mungu huendeleza asili yetu mpya, kutuwezesha kukua katika utakatifu zaidi kwa wakati. Huu ni mchakato unaoendelea wa ushindi mwingi kama vita vya asili mpya na "hema" ambayo hukaa-mtu zamani, asili ya zamani, mwili.

Katika Warumi 7, Paulo anaelezea vita vinavyoendelea kupinga hata watu wenye kukomaa kiroho. Analalama kwamba anafanya asiyopenda kufanya, na kwa kweli, anafanya maovu ambayo huyachukia. Anasema hii ni matokeo ya "dhambi iliyo hai ndani yangu" (Warumi 7:20). Anapendezwa na sheria ya Mungu kulingana na "uhai wake wa ndani," lakini anaona sheria nyingine inayofanya kazi katika " lakini katika viungo vyangu naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi iliyo katika viungo vyangu" (mstari wa 23). Hapa ni mfano maluumu wa vyombo viwili, masharti yoyote ambayo yanaweza kubeba. Jambo ni kwamba vita ni halisi, na ndio moja Wakristo watakapigana nayo maisha yao yote.

Ndio maana waumini wanahimizwa kuua matendo ya mwili (Warumi 8:13), ili kuua kile kinachomfanya Mkristo atende dhambi (Wakolosai 3: 5), na kuweka mbali dhambi zingine kama hasira, ghadhabu , uovu, nk (Wakolosai 3: 8). Yote haya ni kusema kwamba Mkristo ana asili mbili-zamani na mpya-lakini asili mpya inahitaji ufifio endelefu (Wakolosai 3:10). Upyaji huu, bila shaka, ni mchakato wa maisha kwa Mkristo. Ingawa vita dhidi ya dhambi ni vya mara kwa mara, ingawa hatuko chini ya udhibiti wa dhambi (Warumi 6: 6). Kwa kweli, muumini ni "uumbaji mpya" katika Kristo (2 Wakorintho 5:17), na Kristo ndiye hatimaye atatuokoa "kutoka kwenye mwili huu wa kifo." Tunamshukuru Mungu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu!" (Warumi 7: 24-25).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Mkristo ana asili mbili?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries