settings icon
share icon
Swali

Je! Malaika wapo?

Jibu


Biblia inazungumzia malaika kama viumbe halisi. Hata hivyo, taswira ya Maandiko juu ya malaika ni tofauti sana na dhana inayojulikana sana kuwahusu. Biblia inawaelezea malaika kuwa viumbe wenye nguvu nyingi, wenye kuogofya, na wa ajabu. Wanamtumikia Mungu kwa sababu maalum na hawaonekani kuwa viumbe wa kuranda randa au kubahatisha. Ingawa hatuna habari kamili kuhusu malaika katika Biblia, yale yaliyomo yanatosha kurekebisha maoni mengi ya kawaida ambayo ni potovu.

Neno malika linatokana na neno la Kigiriki aggelos (au angelos), ambalo kihalisi humaanisha “mjumbe.” Katika Agano la Kale la Kiebrania, viumbe hawa wanaitwa mal’ak ambalo linamaanisha kitu kile kile “mjumbe.” Katika Biblia mawasiliano yaonekana kuwa kazi kuu ya malaika. Marejeleo mengi inawahusisha wao kutoa habari au amri kwa niaba ya Mungu. Mara kwa mara wanaoneshwa kuwa walinzi wa watu fulani (Danieli 6:20-23) au mataifa (Danieli 12:1). Hata hivyo, hukuna uungwaji wa moja kwa moja wa kibiblia kwa dhana ya “malaika mlinzi”- chombo kimoja cha kiroho kilichopewa mtu binafsi kwa ajili ya ulinzi au mwongozo-ingawa viumbe kama hivyo vinaweza kuwepo.

Katika siku hizi, ishara ya kawaida ya malaika inajumuisha vitu kama vile nuru, mbawa za manyoya, nywele za kimanjano, vinubi, na mavazi meupe, au watoto wachanga walio na mabawa ndogo na macho yanayong’aa. Kwa kweli, Biblia haitupi maelezo kamili ya vile malaika wanaonekana kwa mwili. Ni aina chache tu za viumbe maalum, kama vile makerubi na maserafi, wanapewa maelezo yao ya moja kwa moja (Isaya 6:2-6; Ezekieli 1:4-28). Ni malaika mmoja tu kwenye kaburi tupu la Yesu, ambaye ameelezewa kuwa amevaa vazi jeupe (Marko 16:5). Maandiko yanaonyesha kwamba malaika wanaweza kuchukua umbo la mwanadamu wa kawaida (Mwanzo 19:1-4).

Hata hivyo, watu wengi katika Maandiko waliokutana na malaika waliitikia kwa hofu. Takribani kila wakati malaika wa Mungu alimtembelea mtu, maneno ya kwanza ya malaika yalikuwa, “usihofu” (Luka 1:13; 2:10; Mathayo 28:5). Uwepo wao unaweza kuwa mwingi, hata mitume kama vile Yohana walipata kuonywa wasiwaabudu (Ufunuo 19:9-10). Hili ni jambo la maana, ukizingatia zile nguvu zinazohusishwa na malaika katika Biblia. Kama viumbe vya kiroho walioumbwa kumtumikia Mungu, malaika wanaonekana sio “maridadi” kama vile wanayo nguvu katika ulimwengu wa kiroho.

Tukitazama Biblia, tunaweza kusema kuwa malaika ni viumbe halisi. Malaika wa Kibiblia wapo. Mifano ya kuigiza ya malaika tunayoiona katika filamu na mapango ya matangazo, kamwe hawapo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Malaika wapo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries