settings icon
share icon
Swali

Je, kanuni ni nini?

Jibu


Neno lililotafsiriwa “kanuni” linamaanisha “agizo, haswa vile linatumika kwa mtindo wa maisha.” Kwa maneno mengine, kanuni ni mafundisho yaliyopitishwa na chanzo chenye mamlaka. Katika Biblia, neno hilo siku zote hurejelea nyanja inayohusu Kiroho. Biblia inasema kuhusu yenyewe kwamba “lafaa kwa mafundisho,na kwa kuwaonya watu makossa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki” (2 Timotheo 3:16). Tunahitaji kuwa waangalifu kuhusu kile tunaamini na kuwakilisha kama ukweli. 1 Timotheo 4:16 inasema, “Jitunze nafsi yako, na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia.”

Kanuni ya Kibiblia hutusaidia kuelewa mapenzi ya Mungu kwa maisha yetu. Kanuni ya Kibiblia hutufundisha asili na tabia ya Mungu (Zaburi 90:2; 97:2; Yohana 4:24), njia ya wokovu kupitia imani (Waefeso 2:8-9; Warumi 10:9-10), maagizo kwa kanisa (1 Wakorintho 14:26; Tito 2:1-10), na viwango vya Mungu vya utakatifu juu ya maisha yetu (1 Petro 1:14-17; 1 Wakorintho 6:18-20). Wakati tunakubali Biblia kama Neno la Mungu kwetu (2 Timotheo 3:16; 2 Petro 1:20-21), tuna msingi imara kwa kanuni yetu. Kunaweza kuwa na kutoelewana ndani ya mwili wa Kristo juu ya hoja sisizo za msingi wa kanuni, kama vile mafundisho ya siku za mwisho (eskatolojia), shirika la kanisa, au karama ya Roho Mtakatifu. Lakini mafundisho ya kibiblia ya kweli ni yale ambayo yanajumuisha “kusudi lote la Mungu” (Matendo ya Mitume 20:27) na kuleta hitimisho kupitia yale ambayo yanaonekana yanaegemea kwa karibu sana na tabia ya Mungu wetu asiyebadilika (Hesabu 23:19; Waebrania 13:8).

Hata hivyo, kila wakati Biblia sio msingi ambao watu au makanisa hujenga kauli zao za kanuni. Asili yetu ya dhambi haitii kwa urahisi amri za Mungu, hivyo mara kwa mara tunachagua sehemu ya Biblia ambazo hutufurahisha na kutupa zingine. Au tunabalisha kile Mungu anasema na mafundisho yaliyotengenezwa na binadamu au tamaduni. Hili sio jambo geni. Yesu aliwakemea waandishi na Mafarisayo kwa “mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu” (Marko 7:7; cf. Isaya 29:13). Mafundisho ya uwongo yalieenea wakati wa Agano Jipya, na Maandiko yanatuambia yataendelea kuwapo (Mathayo 7:15; 2 Petro 2:1; 1 Yohana 4:1). 2 Timotheo 4:3 inasema, “Maana wakati utakuja watu watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kuyasikia.”

Biblia inatoa onyo kali kwa wale ambao wanaeza fundisha mafundisho ya uwongo au yasiyokamilifu kwa sababu yanalingana na mawazo ya binadamu. 1 Timotheo 6:3-4 inasema, “Ikiwa mtu yeyote atafundisha mafundisho mapotovu wala hakubaliani na mafundisho manyofu ya Bwana wetu Yesu Kristo na yale ya utauwa, huyo amejivuna wala hajui kitu chochote.” Mtume Pauli aliandika maneno kali kuhusu kuipotosha injili na mafundisho ya uwongo: “ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo. 8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele! 9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!” (Wagalatia 1:7-9).

Mafundisho ni mtazamo wa ulimwengu jinsi tunavyojiongoza maisha yetu. Ikiwa mafundisho yetu yako juu ya msingi wa Maandiko, tunaweza jua tunatembea katika njia ambayo Mungu alitukusudia. Hata hivyo, ikiwa hatutasoma Neno la Mungu sisi wenyewe (2Timotheo 2:15), tunaongozwa kwa hurahisi katika makosa. Ingawa kuna masuala machache mbalimbali ambayo Wakristo wanatofautiana, mafundisho ya kweli ni wazi Zaidi kuliko vile wengi wanadokeza. 2 Petro 1:20 inasema kwamba “Zaidi ya yote, yawapasa mjue kwamba hakuna unabii katika Maandiko uliofasiriwa kama alivyopenda nabii mwenyewe.” Kuna haki ya kufasiri kila kitu Mungu anasema, na ni jukumu letu kutambua maana hiyo, sio kuunda tafsiri ambayo inafaa mawazo yetu. Mungu anataka tujue moyo Wake na ametupa Neno Lake ambalo juu yake tutajenga maisha ya kimungu (ona Mathayo 7:24). Tunapojifunza zaidi mafundisho ya kweli, tunamweelewa Mungu zaidi na hata sisi wenyewe.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, kanuni ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries