settings icon
share icon
Swali

Je, tutalala mbinguni?

Jibu


Usingizi ni hitaji la kimwili kwa miili yetu ya duniani. Bila usingizi, ubongo wetu huacha kufanya kazi kwa usahihi, na miili yetu inakataa kushirikiana. Mzunguko wa kuamka na kulala ni mwingine tu kati ya miandamo mingi ambayo Mungu anaweka duniani-miandamo mingine inatia ndani miduara ya mabadiliko ya majira, mchana na usiku, na mzunguko wa maji. Mizinguko hii ni sehemu ya maisha kwenye sayari hii. Hata hivyo baada ya kifo, tutakuwa katika ulimwengu tofauti. Baada ya kifo, wale walio “ndani ya Kristo” watakuwa pamoja naye mara moja (2 Wakorintho 5:8) lakini bado hawatakuwa na miili yao iliyorejeshwa kabisa. Ni lazima tungojee ufufuo ili kuipokea miili hiyo (1 Wakorintho 15:40; 2 Wakorintho 4:14; Yohana 5:28-29). Kuna uwezekano kwamba, kwa muda, baada ya kifo na kabla ya ufufuo, nafsi zetu hazitahitaji usingizi; badala yake, tutafurahia ibada isiyokoma na furaha katika uwepo wa Bwana.

“Kulala” mbinguni-ulimwengu wa kiroho ambako tunangojea ufufuo-huenda hata kusiwe jambo linalowezekana au la lazima. Yesu alieleza mahali pa kupumzika kwa muda kwa wenye haki kuwa “karibu na Ibrahimu” (Luka 16:23). Tutakuwa na aina fulani ya mwili, na tutatambuana (Luka 16:22-24). Tunaweza kuwa na ujuzi fulani wa mambo duniani (Luka 16:27; Ufunuo 6:9-10). Lakini tunapaswa kuzingatia kwa makini miitikio ya wanadamu waliomwona Mungu katika utukufu Wake kama alivyo fanya Isaya (Isaya 6:1-5), Musa (Kutoka 33:20-23), na Yohana (Ufunuo 1:17). Kuishi katika uwepo dhahiri wa Bwana Mungu Mwenyezi kutabadilisha kila kitu. Mambo ya dunia, ikiwa ni pamoja na usingizi, havitakuwa na thamani ile ile kwetu.

Hata hivyo, Mungu aliumba wanadamu ili wakae katika ulimwengu wa kimwili. Anakusudia kurejesha vitu vyote kuwa vipya (Matendo 3:21). Wakati wa ufufuo roho zetu, ambazo zimekuwa pamoja na Kristo zitaunganishwa tena na miili yetu iliyorejeshwa. Kisha tutakaa katika dunia mpya iliyorejeshwa kabisa pamoja na Yesu (Isaya 65:17; Ufunuo 21:1-2). Umilele utatumiwa tukiishi katika miili mikamilifu katika dunia kamilifu na Yesu akiwa mfalme wetu asiyepingwa. Katika hali ya milele, usingizi unaweza tena kuwa sehemu ya uzoefu wetu, kama vile kula na kunywa (Luka 14:15; Ufunuo 19:9). Lakini usingizi hautakuwa wa lazima kwa sababu ya uchovu au udhaifu kwa sababu miili yetu itakuwa kamilifu kama mwili wa Yesu baada ya kufufuka kwake (Luka 24:41-42). Ukweli ni kwamba hatujui vya kutosha kutoka kwa Maandiko ili kusema kwa uhakika kama tatalala mbinguni au la, katika milenia, au katika hali ya milele. Hilo ni moja ya maelfu ya maswali ambayo tutakuwa tumejibu mbinguni. Jambo moja ambalo ni hakika: tutakapomwona Yesu kwa mara ya kwanza, usingizi utakuwa jambo la mwisho katika akili zetu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, tutalala mbinguni?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries