settings icon
share icon
Swali

Ni nini maana kuwa Eskatolojia ishafanyika?

Jibu


Ugunduaji wa eskatolojia ni nadharia inayoshikilia kwamba vifungu vya kinabii katika Agano Jipya havisungumzii baadaye; badala yake, vinarejelea huduma ya Yesu na “urithi” Wake wa kudumu katika kanisa. Kulingana na utambuaji wa eskatolojia, unabii wote wa Biblia kuhusu ufalme ulitimia wakati wa maisha ya Yesu. Wakati Yesu alisema, “wakati umetimia….. Na ufalme wa Mungu umekaribia” (Marko 1: 15), Alimaanisha kwamba tunahitaji kuelewa ufalme kama majaribio ya kweli yaliopo, badala ya, tukio la baadaye liliko mbali. Utambuaji wa eskatolojia ulianzishwa na mwanatheolojia C. H. Dodd katika kitabu chake cha mwaka wa 1935, Mifano ya Ufalme (The Parables of the Kingdom) na kuwa maarufu kupitia uandishi wake wa baadaye.

Utambuaji wa eskatolojia unasema ya kwamba, matukio ya “baadaye” yaliyotabiliwa katika Biblia sio ya baadaye tena; yalitimizwa yote na Yesu au yanaendelea kutimizwa kanisani. Biblia inasema Masiha atakuja- na Akakuja, wakati Yesu alizaliwa Bethlehemu. Biblia inasema kwamba Mungu atahukumu dhambi za ulimwengu- na Alifanya hivyo, wakati Yesu alikufa msalabani. Biblia inasema ya kwamba waliokufa watafufuka- na wakafufuka, wakati Yesu alifufua Lazaro na wengine kutoka kaburini. Je, itakuaje kuhusu ule unabii wa Biblia kuhusu ujio wa pili, utawala na kutukuka kwa Yesu? Utambuaji wa eskatolojia ushashughulikia hilo, pia- hayo yote yalitimishwa katika ufufuo na kupaa mbinguni kwa Yesu. Eskatolojia ishafanyika.

Kulingana na estakalojia timilifu, usomaji wa eskatolojia hakuhusishi mwisho wa dunia bali “kuzaliwa upya” kwa ulimwengu kwa vile Yesu alivyoweka kiwango na wafuasi Wake wanaendelea kuishi kwa kanuni Zake zisizo na wakati. Watetezi wa dhana kwamba eskatolojia ishafanyika hawangalii mbele kwa unyakuzi, ujio wa pili, au hukumu ya kiulimwengu. Badala yake, wanajaribu kuzingatia yale Yesu alisema na kutenda; mengine yote si muhimu. Kwa njia ingine, utambuaji wa eskatolojia unahusu preterism kamili, mafundisho kwamba unabii wa siku za mwisho katika Biblia umetimizwa; na theolojia ya “Ufalme Sasa”, inayosema ya kwamba tayari tunaishi katika ufalme wa Mungu na tunaeza guza ahadi zinazohusishwa na ufalme wakati wowote tunataka.

Ukweli kwamba eskatolojia ishafanyika uliazishwa na mwanatheolojia apendaye fikra mabadiliko- na unaendelea kuwa mafundisho bembelezi miongoni mwa wapendao fikra za mabadiliko inatosha kutupatia onyo. Lakini muhimu Zaidi kuliko hilo ni kulinganisha mafundisho ya kuwa estakolojia ishafanyika na yale Biblia inasema pamoja na yale tunayojua kuwa ya kweli kuhusu matukio ya ulimwengu. Bila shaka, kuna vipengele fulani vya eskatolojia ambavyo “vimeshatukia” au kutimizwa. Lakini sio kila kitu. Yesu Mwenyewe alisema “maisha haya… milele ujao” (Luka 18:30), akiwapatia wanafunzi Wake matumaini ya ulimwengu ujao ambao ni tofauti na uliopo. Wakati Yesu alipaa mbinguni, malaika waliwambia wanafunzi, “Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni” (Acts 1: 11). Maneno ya malaika bado yanaonyesha wazi kwa matukio ya baadaye ya eskatolojia, hii ikiwapatia wanafunzi kitu cha kutumainia (ona Tito 2:13).

Wakati Yesu alisema, “Ufalme wa Mungu umekaribia” (Marko 1:15), hakuwa Anasema kwamba alikuwa anatimiza unabii wote kwa wakati huo. Badala yake, Yesu alikuwa anatibitisha ushahidi kuwa Yeye alikuwa ndiye Masiha. Wakati wowote Yesu alinena na kutenda katika nguvu za Mungu, ufalme kwa kweli ulikuwa “umefika”; kila wakati Yesu aliponya mtu kilema au kutoa pepo, mbingu ilikuwa inaguza ulimwengu. Yesu alikuwa atoa onjo ya vitu vya ajabu vitakaokuja katika ufalme wa Mungu. Immanueli hakika alikuja kulipia Israeli iliyotekwa.

Kulikuwa na ahadi ambazo zilihusishwa na kuja kwa Yesu ambazo hazikutimia katika tangazo Lake la kwanza. Bwana Mwenyewe anathibitisha hili katika Luka 4. Wakati Yesu alisimama na kusoma kutoka Isaya katika sinagogi ya Nazareti, Anatangaza kuhitimizwa kwa nabii kadhaa za kimasiha: Anatangaza ujumbe mpya kwa masikini, anatoa uhuru kwa wafungwa na kurejesha kuona kwa vipofu, anafungulia waliodhulumiwa, na kutangaza mwaka wa Bwana wenye fadhili (Luka 4:18-19; Isaya 61:1-2). Lakini Yesu aliachia kusoma njiani na kumkabidhi muhudumu ile hati alikuwa anasoma kwayo. “Leo hii”, Yesu anasema, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia” (Luka 4:21). Yesu hakuwa amesoma maandiko hayo yote. Kulikuwa sehemu zingine za eskatolojia ya Isaya ambazo hazikutimia siku hiyo, kama vile,”siku ya kisasi ya Mungu wetu” (Isaya 61:2). Kitu kingine kikuu kilikuwa kimeahidiwa, kitu ambacho Yesu alikiacha kikitimizwa siku ingine. Kwa maneno mengine, Yesu alifundisha eskatolojia ambayo “haijatimizwa”.

Kuna mambo mengi yaliyotabiliwa katika Biblia ambayo hayajatimia. Tunangojea kutimizwa kwao katika kuweka tumaini kwamba Mungu ni mwaminifu na hawezi kudanganya. Kujaribu kufafanua unabii wa kibiblia kuwa sio halisi, hii ikiwa ndio dhana eskatolojia timilifu inafanya, inaenda kinyume na kanuni zuri ya tafsiri ya kibiblia.

English

Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni nini maana kuwa Eskatolojia ishafanyika?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries