settings icon
share icon
Swali

Ni nini maana ya kuachana na kushikamana?

Jibu


"Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ne ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja" (Mwanzo 2:24). Tafsiri nyingine hutoa "kuachana na kuambatana" kama "kuachana na kuungana", "kuachana na kushikana", na "kuondoka na shikamaneni". Hivyo, ni nini hasa maana ya kuachana na baba yako na mama yako na kuambatana na mke wako?

Kama kumbukumbu katika Mwanzo sura ya 2, Mungu alimuumba Adamu wa kwanza, na Hawa baadaye. Mungu mwenyewe alimleta Hawa kwa Adamu. Mungu mwenyewe aliamuru kwamba wataunganishwa pamoja katika ndoa takatifu. Alisema kuwa wawili hao watakuwa mwili mmoja. Hii ni picha ya uchumba katika ndoa tendo hilo la upendo kamwe halifai kuhusisha mtu mwingine yeyote. Na "kushikamana" ina maana yake "kuambatana na, fimbo, au kujiunga na." Ni ya kipekee ya kujiunga na ya watu wawili katika mwili mmoja. Ina maana kuwa sisi hatutoroki wakati mambo hayatwendei salama. Ni pamoja na kuzungumza mambo kwa wazi, na kuomba muda huo wote, kuwa na subira na matumaini kuwa Mungu atafanya kazi katika yenu mioyo wawili, kuwa tayari kukubali unapokuwa na makosa na kuomba msamaha, na kutafuta mashauri ya Mungu mara kwa mara katika neno lake.

Kama mmoja wa wanaharusi atashindwa kuachana na kuambatana, matatizo yatatokea katika ndoa. Kama mwanandoa hukataa kweli kuacha wazazi, mgogor na matatizo yatatokea. Kuacha wazazi wako haina maana kuwapuuza au kukosa muda wowote pamoja nao. Kuacha wazazi wako ina maana kwamba unatambua kuwa ndoa yako imeanzisha familia mpya na kwamba familia hii mpya lazima ipewe kipaumbele kuliko familia yako zamani. Kama wanandoa watapuuza kushikamana pamoja, matokeo yake ni ukosefu wa urafiki na umoja. Kuambatana na mke wako haina maana kuwa kushinda naye kila wakati au kukosa kuwa na urafiki wa maana nje ya ndoa yako. Kuambatana ina maana kuwa unatambua kwamba wewe umeunganika, kimsingi "kushikanishwa" kwa mume/.mke wako. kuambatana ni muhimu katika kujenga ndoa ambayo huvumilia nyakati ngumu na kuwa na uhusiano mzuri ambao Mungu anakusudia.

"Kuachana na kuambatana" katika ukaribu wa ndoa ni picha ya muungano ambao Mungu anataka tuwe naye. "Tembeeni kwa kumfuata Bwana Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye" (Kumbukumbu 13:4). Ina maana kuwa tuachane na miungu mingine yote, mtindo wowote inaweza chukua, na kujiunga na yeye peke yake kama Mungu wetu. Tushikamane na yeye kama viel tunaposoma neno lake na kujiwasilisha kwa mamlaka yake juu yetu. Basi, tunapomfuata kwa karibu, tunaona kwamba maagizo yake kuacha baba na mama ili kushikamana na wenzi wetu ni kugundua ahadi na usalama, kama vile alivyokusudia. Mungu anachukulia ubuni wake wa ndoa kwa umakini sana. Kuachana na kuambatana ni mpango wa Mungu kwa wale ambao huoa. Wakati tunafuata mpango wa Mungu, sisi ni kamwe hatutaibishwa.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni nini maana ya kuachana na kushikamana?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries