settings icon
share icon
Swali

Je! Ninawezaje kupata faraja wakati mpendwa ambaye hajaokoa amekufa?

Jibu


Kwa muumini, kifo cha mpendwa ambaye hajaokoka ni kigumu sana. Wakati mwingine inaonekana hatutapata faraja au amani ya akili tunapojua hatima inayowangojea wasiookolewa. Mpendwa wetu aliyeokoka anapokufa, tunamkosa, lakini hatuhuzuniki “kama watu wengine wasiokuwa na tumaini” (1 Wathesalonike 4:13), kwa sababu tunajua tutaunganika siku moja mbinguni.

Lakini kwa wale wanaokufa bila Kristo, tunajua hatutawaona tena, na kupata faraja katika hali hiyo ni vigumu sana.

Hasa kwa wale ambao wamejitahidi sana kuwasilisha kweli za Injili kwa wapendwa wao, kuna kuhusishwa na hali hii ya maumivu ambayo inauliza ni “kwa nini?” tukiwa Wakristo, tunashangaa jinsi mtu yeyote angeweza kukataa zawadi hiyo yenye thamani. Shangwe yetu katika Bwana hutusukuma kuwatakia wengine shangwe hiyohiyo. Hata hivyo, ukweli ni kwamba ingawa mwaliko huo uko wazi kwa wote, wengine hawatapokea zawadi. Lakini tunaweza kupata faraja, kitia-moyo, na uhakikisho katika kweli kwamba ingawa huenda hatutamuona tena mpendwa wetu, sikuzote Mungu ni mwaminifu na mwenye haki. Inashangaza kuelewa kwamba Mungu ni mvumilivu sana na ameuacha mlango wazi kwa muda mrefu sana.

“Je, Mwamuzi wa dunia yote hatafanya lililo sawa” (Mwanzo 18:25)? Hii ni faraja kubwa kwa wengi wetu walio na wapendwa ambao wameaga na hatuna uhakika wa hatima ya roho zao. Mungu ni Hakimu mkuu wa haki, amejawa neema na rehema kwa wote wamwitao. Ni haki yake yenyewe inayotoa “njia” kwa ajili ya wote kuepuka hukumu ya haki yake, na ni katika haki hiyo kwamba ni lazima tupumzike. Ni neema inayotuokoa, na ni neeema ambayo inatupasa kusimama tunapopitia majonzi maradufu ya kifo cha mpendwa ambaye hajaokoka. Ni lazima tukumbuke kwamba hatuwezi kufanya uchaguzi huu kwa ajili ya mtu mwingine yeyote, na kama waliingia katika umilele bila Kristo, hilo lilikuwa chaguo lao licha ya toleo la neema.

Ingawa tunaweza kuwa na uchungu katika kumbukumbu ya mpendwa huyo tukiwa katika maisha haya na kupitia mchakato wa huzuni, wakati utakuja ambapo kila muumini aliyezaliwa mara ya pili atakuwa pamoja na Bwana. Katika siku hiyo “Atafuta kila chozi kutoka macho yao. Mauti haitakuwepo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu, kwa maana mambo ya kwanza yamekwisha kupita” (Ufunuo 21:4). Hatuwezi kuelewa jinsi hiyo itakavyokuwa kwa sababu tunaishi katika wakati na tumebanwa na akili zetu zenye kikomo. Hata hivyo, kuwaza tu hilo kunatosha kuleta faraja na kiutia moyo. Tutakapomwona Bwana, huzuni yote tuliyo nayo sasa itatoweka. “Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye” (Yohana 16:22). Kwa wakati huu, tunaweza kuegemea mabawa ya milele ya Mungu, ambaye huhisi uchungu wetu na kutufariji kwa upendo na huruma Yake kuu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Ninawezaje kupata faraja wakati mpendwa ambaye hajaokoa amekufa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries