settings icon
share icon
Swali

Je, uroho ni dhambi? Biblia inasema nini juu ya ulaji kupita kiazi?

Jibu


Ulafi unaonekana kuwa dhambi kwamba Wakristo hupenda kupuuza. Sisi mara nyingi huwa wepesi kutaja uvutaji sigara na ulevi kuwa dhambi, lakini kwa baadhi ya sababu uroho unaitikiwa au kuvumiliwa. Wengi wa hoja zinazotumiwa dhidi ya kuvuta sigara na kunywa, kama vile afya na madawa ya kulevya, pia zinatumika kwa kula kupita kiasi. Waumini wengi hawachukulii kobo la mvinyo au uvutaji sigara kuwa jumbo kubwa, lakini hawana wasiwasi kuhusu kuvimbiwa katika meza ya sherehe ya chakula cha jioni. Hii haipaswi kuwa hivyo!

Mithali 23:20-21 anatuonya, "Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; miongoni mwao walao nyama kwa pupa. Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, na utepetevu humvika mtu." Mithali 28:7 inasema, "Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye hekima; bali aliye rafiki wa walafi humbaibisha babaye. "Mithali 23:2 anatangaza," Jitie kisu kooni kam ukiwa mlafi. "

Hamu ya kimwili ni mfano wa uwezo wetu wa kujidhibiti wenyewe. Kama sisi hatuwezi kuidhibiti tabia yetu ya kula, hivyo basi hatuwezi kudhibiti tabia a wengine, kama vile wale wa akili ya (tamaa, ona shauku, hasira) na hawawezi kuzuia midomo yao na uvumi au ugomvi. Hatupaswi kuruhusu hamu zetu kututawala, bali tunafaa kuwa udhibiti kwa hamu zetu. (Angalia Kumbukumbu 21:20, Mithali 23:2, 2 Petro 1:5-7, 2 Timotheo 3:1-9, na 2 Wakorintho 10:5). Uwezo wa kusema "hapana" na kitu chochote zaidi ya ziada ni udhibiti wa binafsi -na moja ya matunda ya Roho ambayo ni kawaida kwa waumini wote (Wagalatia 5:22).

Mungu ametubariki kwa kujaza dunia na vyakula vya ladha, lishe, na utamu. Tunapaswa kuheshimu viumbe wa Mungu na kufurahia vyakula hivi na kwa kuvila kwa njia sahihi. Mungu anatuita kudhibiti matumizi ya chakula yetu, badala ya kuiruhusu itudhibiti.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, uroho ni dhambi? Biblia inasema nini juu ya ulaji kupita kiazi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries