settings icon
share icon
Swali

Je, Biblia inasema nini kuhusu kutokuwa na nyege?

Jibu


Kifiziolojia, siojinsi inafafanuliwa kuwa “kutokuwa na jinsia dhahiri au viungo vya ngono; bila jinsia.” Walakini, kwa kawaida, ukosefu wa nyege, unapozungumziwa, unarejelea “kukosa hamu ya ngono.” Kwa kuwa hakuna mahali Biblia inataja hali ya jinsia ya kifiziolojia, kwa madhumuni ya nakala hii, tutashughulikia pekee ukosefu wa mvuto au hamu ya ngono. Je, ni makosa kutokuwa na hamu/mvuto wowote wa tendo la ndoa?

Kile ambacho Paulo anaandika katika 1 Wakorintho 7 ni jambo linalokaribiana sana kwa kutajwa kwa kibiblia juu ya ukosefu wa nyege. Katika mstari wa 1 anasema ni heri mwanamume asioe. Katika nyakati za useja, bila vikwazo vya familia, mtu anaweza kuwa na wakati ili kutumiwa na Mungu mahali popote na wakati wowote. Kinyume chake, katika mistari ya 2-6, Paulo anaandika kwamba ndoa ni nzuri kwa wale ambao wana mapenzi makali kwa jinsia tofauti. Ndoa huruhusu tamaa hiyo kutimizwa kwa njia ya kimungu. Kisha Paulo anaweka wazi katika mistari ya 7-8 kwamba, hakuwa ameoa wakati huo. Mungu alikuwa amempa Paulo zawadi ya useja, uwezo wa kuwa mseja kwa furaha na kutosheka. Je, hii ina maana kwamba Paulo hakuwa na hamu kabisa ya ngono/au hakuwa na hamu ya kuoa? Sio lazima, lakini vyovyote vile, tamaa ya Paulo kwa wazi haikuzidi ile ya kumtumika Mungu. Kumbuka katika 1 Wakorintho 9:5, Paulo labda anaonyesha hamu ya kuoa.

Kwa hiyo, ni makosa kwa mtu kukosa hamu ya kuoa au kuolewa? Kulingana na 1 Wakorintho 7, hapana, hakika si vibaya. Kubaki mseja kunaweza kuwa jambo zuri sana, kwa kuwa kunaweza kumweka huru mtu ili awe na wakati mwingi zaidi wa kumtumikia Mungu. Hata hivyo, kubaki mseja haimaanishi ukosefu wa nyege, yaani, kukosa hamu ya kuwa na watu wa jinsia tofauti. Zawadi ya useja inayotajwa katika 1 Wakorintho 7 ni uwezo wa kuridhika bila ndoa, na sio lazima kukosa tamaa yoyote ya ndoa. Ikiwa mtu hana hamu ya ndoa/ngono, na ana uhakika kwamba hii ni ya Bwana, anapaswa kutumia wakati wake wa useja kwa kumtumkia kwa moyo wote katika ufalme wa Mungu. Haitakuwa mbaya, hata hivyo, kutafuta ushauri wa matibabu, ili kuhakikisha kuwa kukosa nyege sio kwa sababu ya homoni kutolingana uzito.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, Biblia inasema nini kuhusu kutokuwa na nyege?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries