settings icon
share icon
Swali

Ina maana gani kwamba Mungu ni baba wa mayatima?

Jibu


Zaburi ya 68: 5 inasema, "Baba ya yatima, mtetezi wa wajane, ndiye Mungu katika makao yake matakatifu." Kwa njia zote Bwana Mungu Mwenye Nguvu angeweza kuchagua kujihusisha na ubinadamu, alichagua lugha ya familia . Angeweza kujieleza Mwenyewe kama dikteta mwenye huruma, bosi mwenye wema, au mwenye nyumba mvumilivu. Lakini badala yake, alichagua neno baba.

Anajionyesha Mwenyewe kama Baba kwa sababu sisi wote tunajua baba ni nani na kenye anafanya. Hata kama hatuna baba wa kidunia ambao walitulea vizuri, tuna ufahamu wa ndani wa kenye baba mzuri anapaswa kuwa. Mungu alipanda ufahamu huo ndani ya mioyo yetu. Sisi sote tunahitaji kupendwa, kushangiliwa, kulindwa, na kuhesabiwa ka thamani. Kwa kweli, baba wa kidunia atakutana na mahitaji hayo. Lakini hata kama hana, Mungu atakuwa. Yesu aliwafundisha wafuasi wake kuwasiliana na Mungu kama Baba (Luka 11: 2). Katika Maandiko, Mungu anaelezea upendo wake kwetu kama ule wa mzazi mwenye kujali (Isaya 49:15, Yohana 16: 26-27; 2 Wakorintho 6:18). Ingawa ana sifa za baba na mama (Isaya 66:13), anachagua neno la kiume kwa maana pia linaashiria nguvu, ulinzi, na utoaji (Zaburi 54: 4).

Mungu ana nafasi maalum katika moyo Wake kwa yatima na wasio na baba (Kumbukumbu la Torati 24:20; Yeremia 49:11; Yakobo 1:27). Zaburi 27:10 inasema, " Baba yangu na mama yangu wameniacha, Bali Bwana atanikaribisha kwake." Mungu anajua kwamba mara nyingi baba wa kidunia hawako au hawajafanya kazi zao (Waefeso 6: 4). Anatoa kujaza nafasi ya Baba (Yohana 6:37; Kumbukumbu la Torati 1:31). Anatualika kumwita wakati tunapokuwa na shida (Zaburi 50:15), kutupa wasiwasi wetu wote juu yake (1 Petro 5: 7), na kufurahia kampuni yake (1 Wakorintho 1: 9: Zaburi 116: 1; 1 Yohana 5:14). Anatuonyesha sifa ambazo alikuwa na mawazo wakati alipokuwa ameumba baba. Ingawa mara nyingi baba wa kidunia hawaishi kulingana na kile kinachofaa, Mungu anaahidi kwamba, ndani yake, hakuna mtu anayepaswa kuwa na Baba mkamilifu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ina maana gani kwamba Mungu ni baba wa mayatima?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries