settings icon
share icon
Swali

Ninawezaje kujitayarisha kwa ndoa?

Jibu


Mtu kujitayarisha kwa ndoa kibibilia ni sawa na kujitahidi katika maisha. Kuna kanuni ambayo inastatahili kuongoza sehemu zote za maisha yetu kama Wakristo ambao tumeokoka: “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote” (Mathayo 22:37). Hii si amri ya mzaa. Ndio nguzo ya katikati ya maisha yetu kama Wakristo. Ni kuchagua kumtazamia Mungu na neno lake kwa moyo wetu wote ili nafsi zetu na akili zetu zijazwe na mambo ambayo yanamfurahisha Mungu.

Uhusiano tukonao na Mungu kupitia kwa Yesu Kristo ndio unaweka uhusiano wote katika mtazamo. Uhusiano wa ndoa umejengwa juu ya mfano wa Kristo kwa Kanisa lake (Waefeso 5:22-33). Kila sehemu ya maisha yetu inaongozwa na bidii yetu kama Wakristo kuishi kulingana na amri na sheria za Mungu. Utiifu wetu kwa Mungu na neno lake unatuami kutimiza majukumu yetu ambayo tumepewa na Mungu katika ndoa na neno lake. Na jukumu la kila Mkristo ambaye ameokoka ni kumtukuza Mungu kwa mambo yote (1 Wakorintho10:31).

Ili tujitayarishe kwa ndoa, tutembea kadiri na mwito wetu katika Kristo Yesu, na tuwe na ushirika wa karibu na Mungu kupitia kwa neno lake (2 Timotheo 3:16-17), tazamia utiifu katika mambo yote. Hakuna mpango rahisi wa kujifunza kutembea kwa utiifu kwa Mungu. Ni chaguo ambalo ni lazima tulifanye kila siku tuweke kando mitazamo ya kiulimwengu na badala yake tumufuate Mungu. Kutembea kadri na namna Yesu alitembea na kujitoa kwa unyenyekevu kwa njia moja peke, njia peke ya kweli na maisha peke siku baada ya siku, wakati hadi wakati. Huko ndiko kujiandaa kila Mkristo anastahili kujitayarisha kwa zawadi ambayo twaiita ndoa

Mtu ambaye amekomaa kiroho na anatembea na Mungu amejitayarisha kwa ndoa kuliko kitu kingine kile. Ndoa huitaji jitiada, hisia, unyenyekevu, upendo na heshima. Hizi tabia kila mara zajidhihirisha kwa mtu ambaye ako na uhusiano wa karibu na Mungu. Unapojitayarisha kwa ndoa, tazamia kumruhusu Mungu akuchonge na akufinyange uwe mume au mke anayetaka uwe (Warumi 12:1-2). Ukinyenyekea kwake, atakuwezesha uwe tayari kwa ndoa wakati siku hiyo ya ajabu ikiwadia.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ninawezaje kujitayarisha kwa ndoa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries