settings icon
share icon

Kitabu cha Wagalatia

Mwandishi: Wagalatia 1: 1 anatambulisha wazi Mtume Paulo kama mwandishi wa Waraka kwa Wagalatia.

Tarehe ya kuandikwa: Kulingana na pale hasa kitabu cha Wagalatia kilitumwa na wakati gani wa safari ya kimisionari Paulo alianzisha makanisa katika maeneo hayo, kitabu cha Wagalatia kiliandikwa mahali fulani kati ya 48 na 55 BK

Kusudi la Kuandika: Makanisa ya Galatia yaliundwa na baadhi ya Wayahudi waliookoka na baadhi ya Mataifa waliookoka, kama ilivyokuwa suala kwa ujumla. Paulo anadai tabia yake ya kitume na mafundisho aliyofunza, ili apate kuthibitishia makanisa ya Galatia katika imani ya Kristo, hasa kulingana na hoja muhimu ya kuhesabiwa haki kwa imani peke yake. Hivyo dhamira ni sawa na ile ambayo imejadiliwa katika barua kwa Warumi, yaani, kuhesabiwa haki kwa imani peke yake. Katika waraka huu, hata hivyo, makini imeelekezwa kwa hoja kwamba watu wanahesabiwa haki kwa imani pasipo na matendo ya sheria za Musa.

Wagalatia halikuandikwa kama insha katika historia ya kisasa. Ilikuwa maandamano dhidi ya kupotosha injili ya Kristo. Ukweli halisi wa kuhesabiwa haki kwa imani badala ya kwa matendo ya sheria ulikuwa umezuiwa na kusisitiza kwa Wayahudi kwamba waumini katika Kristo lazima waitii sheria ikiwa walitarajia kuwa kamilifu mbele za Mungu. Wakati Paulo aligundua kwamba mafundisho hayo yalikuwa yameanza kuingia katika makanisa ya Galatia na kwamba yalikuwa yamewatenganisha kutoka kwa urithi wao wa uhuru, aliandika ulalamikaji wenye hamaki ulio katika waraka huu.

Mistari muhimu: Wagalatia 2:16: "hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo,wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki. "

Wagalatia 2:20: "Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu . "

Wagalatia 3:11: "Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu, 'Mwenye haki ataishi kwa imani."

Wagalatia 4: 5-6: "kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana. Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani,Baba. "

Wagalatia 5: 22-23: "Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; Juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. "

Wagalatia 6: 7: "Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna."

Muhtasari kwa kifupi: Matokeo ya kuhesabiwa haki kwa neema kwa njia ya imani ni uhuru wa kiroho. Paulo alitoa wito kwa Wagalatia kusimama imara katika uhuru wao, na "wasiingie tena kwa nira za utumwa (yaani, sheria ya Musa)" (Wagalatia 5: 1). Uhuru wa Kikristo si udhuru wa kufurahisha asili ya chini ya mtu; badala yake, ni nafasi ya kupendana (Wagalatia 5:13; 6: 7-10). Uhuru kama huo hufedheheshi mtu kutoka kwa mapambano ya maisha. Hakika, unaweza kuimarisha vita kati ya Roho na mwili. Hata hivyo, mwili (asili ya chini) umesulubiwa pamoja na Kristo (Wagalatia 2:20), na, kama matokeo, Roho itazaa matunda yake kama vile upendo, furaha, na amani katika maisha ya muumini (Wagalatia 5: 22-23).

Barua kwa Wagalatia iliandikwa katika roho iliyotiwa msukumo uliochochewa. Kwa Paulo, suala halikuwa kama mtu ametahiriwa, bali kama alikuwa amekuwa"kiumbe kipya" (Wagalatia 6:15). Ikiwa Paulo hakuwa amefaulu katika majadiliano yake kwa kuhesabiwa haki kwa imani pekee, Ukristo ungalibakia dhehebu ndani ya Uyahudi, badala ya kuwa njia ya wokovu kwa wote. Wagalatia, kwa hivyo, si tu waraka wa Lutha; ni waraka wa kila muumini ambaye anakiri na Paulo: "Nimesulubiwa pamoja na Kristo, lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu "(Wagalatia 2:20).

Vitabu vya Yakobo na Wagalatia vinaonyesha mambo mawili ya Ukristo ambayo tangu mwanzo yameonekana kuwa katika vita, ingawa katika hali halisi ni ya ziada. Yakobo anasisitiza juu ya maadili ya Kristo, mahitaji kwamba imani ithibitishe uwepo wake kwa matunda yake. Hata hivyo Yakobo, si chini ya Paulo, anasisitiza haja ya mabadiliko ya mtu binafsi kwa neema ya Mungu (Yakobo 1:18). Wagalatia inasisitiza nguvu ya injili ambayo inazalisha maadili (Wagalatia 3: 13-14). Wala Paulo si eti hakujali kuliko Yakobo kuhusu maisha ya kimaadili (Wagalatia 5:13). Kama pande mbili za sarafu, mambo haya mawili ya ukweli wa Kikristo lazima daima yaambatane.

Mashirikisho: Katika Waraka wote wa Paulo kwa Wagalatia, neema ya kuokoa -zawadi ya Mungu- imewekwa sambamba dhidi ya sheria ya Musa, ambayo haiokoi. Wayahudi, wale ambao wangerudi kwa sheria ya Musa kama chanzo chao cha kuhesabiwa haki, walikuwa maarufu katika kanisa la kwanza, hata kwa muda kuvutia Mkristo maarufu kama Petro katika mtandao wao wa udanganyifu (Wagalatia 2: 11-13). Hivyo ndivyo Wakristo wa kwanza walikuwa wameambatishwa kwa sheria ambayo Paulo aliendelea kurudia ukweli kwamba wokovu kwa neema haukuhusiana na kutii sheria. Dhamira zinazounganisha Wagalatia kwa Agano la Kale zililenga kwa sheria dhidi ya neema: kutokuwa na uwezo kwa sheria kuhesabiwa haki (2:16); ufu wa muumini kwa sheria (2:19); Ibrahimu kuhesabiwa haki kwa imani (3: 6); sheria haileti wokovu bali ghadhabu ya Mungu (3:10); na upendo, si matendo, hutimiliza sheria (5:14).

Vitendo Tekelezi: Mojawapo ya dhamira kuu za kitabu cha Wagalatia hupatikana katika 3:11: "Mwenye haki ataishi kwa imani." Sio tu kwamba sisi huokolewa kwa imani (Yohana 3:16; Waefeso 2: 8-9), bali maisha ya muumini katika Kristo - siku kwa siku, wakati kwa wakati - huishiwa kwa na kupitia kwa imani hiyo. Si kwamba imani ni kitu tunabuni kwetu wenyewe-ni zawadi ya Mungu, si ya matendo-lakini ni wajibu wetu na furaha (1) kudhihirisha imani yetu ili wengine waone kazi ya Kristo ndani yetu, na (2) tuzidishe imani yetu kwa kutekeleza masomo ya kiroho (kujifunza Biblia, maombi, utiifu).

Yesu alisema tutajulikana kwa matunda ya maisha yetu (Mathayo 7:16) ambayo yanatoa ushahidi wa imani iliyo ndani yetu. Wakristo wote wanatakiwa kuwa wenye bidii katika kujitahidi kujijenga juu ya imani ya kuokoa iliyo ndani yetu ili maisha yetu yamashirie Kristo na wengine watamwona ndani yetu na "wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni" (Mathayo 5:16, NKJV).

English

Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kitabu cha Wagalatia
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries