settings icon
share icon

Kitabu cha 3 Yohana

Mwandishi: kitabu cha 3 Yohana hakimtaji mwandishi wake moja kwa moja. Utamaduni kutoka siku za mwanzo za kanisa umekuwa kwamba mtume Yohana ndiye mwandishi. Kumekuwa na tuhuma mara kwa mara kutoka kwa wale ambao walidhani inawezekana kwamba hii iliandikwa na mwanafunzi wa Bwana mwingine aitwaye Yohana, lakini ushahidi wote unaelekezwa kwa mwandishi kuwa Yohana.

Tarehe ya kuandikwa: kitabu cha 3 Yohana huenda kiliandikwa wakati mmja na ule wa barua zingine za Yohana, Yohana ya 1 na 2, pengine kati ya 85-95 BK.

Kusudi la Kuandika: lengo la Yohana katika kuandika barua hii ya tatu ni ushahidi wa mara tatu. Kwanza, anaandika kuwasifu na kuwatia moyo wapenzi wafanyakazi wenzake, Gayo, katika huduma yake ya ukarimu kwa wajumbe wa kuzungukazunguka ambao walikuwa wanakwenda kutoka sehemu maja hadi nyingine kuhubiri Injili ya Kristo. Pili, anaonya na kulaani kwa njia isiyo ya moja kwa moja tabia ya Diotrefe, kiongozi wa kidikteta ambaye alikuwa amenyakua kanisa moja katika jimbo la Asia, na ambaye tabia yake ilipingwa moja kwa moja kwa wote ambao mtume na Injili yake ilisimama kwao. Tatu, anasifu mfano wa Demetrio ambaye aliripotiwa kuwa na ushuhuda mzuri kuliko wote.

Mistari muhimu: 3 Yohana 4: "Sina furaha iliyo kuu kuliko hii, kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli"

3 Yohana 11: "Mpenzi, usiuige ubaya, bali uige wema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu, bali yeye atendaye mabaya hakumwona Mungu."

Muhtasari kwa kifupi: Yohana anaandika kwa msisitizo wake wa kawaida wa nguvu juu ya ukweli kwa huyu ndugu mpendwa sana katika Kristo, Gayo, mlei/asiye mtaalamu aliye na mali kiasi na mamlaka katika mji uliokuwa karibu na Efeso. Anamsifu sana huduma na ukarimu wa Gayo kwa wajumbe wake ambao misheni yao ilikuwa kuchukua Injili kutoka sehemu moja hadi nyingine, iwapo walijulikana kwake au walikuwa wageni. Yohana anamhimiza kuendelea kutenda mema na asiige mabaya, kama katika mfano wa Diotrefe. Mtu huyu alikuwa amenyakua uongozi wa kanisa katika Asia na si tu alikataa kutambua mamlaka ya Yohana kama mtume lakini pia kupokea barua yake na kuwasilisha kwa maelekezo yake. Pia alisambaza kashfa yenye kijicho dhidi ya Yohana na kuwatenga na kanisa washiriki ambao walitoa msaada na kuonyesha ukarimu kwa wajumbe wa Yohana. Kabla ya kuhitimisha barua yake pia anasifu mfano wa Demetrio, ambaye alikuwa amesikia taarifa bora kumhusu.

Mashirikisho: Dhana ya kuonyesha ukarimu kwa wageni ina vigezo kadhaa katika Agano la Kale. Matendo ya ukarimu katika Israeli ni pamoja na mapokezi ya unyenyekevu na neema ya wageni kwa miji yao kwa ajili ya chakula, malazi na ulinzi (Mwanzo 18: 2-8, 19: 1-8; Ayubu 31: 16-23, 31-32). Aidha, mafundisho ya Agano la Kale yanaonyesha Waisraeli kama watu waliotengwa wanategemea kwa ukarimu wa Mungu (Zaburi 39:12) na Mungu kama Yule aliyetimiza mahitaji yao kwa neema, akiwakomboa kutoka Misri na kuwalisha na kuwavisha katika jangwa (Kutoka 16 , Kumbukumbu 8: 2-5).

Vitendo Tekelezi: Yohana, kama kawaida, anasisitiza umuhimu wa kutembea katika ukweli wa Injili. Ukarimu, msaada na kutia moyo kwa Wakristo wenzetu ni moja ya maadili muhimu ya mafundisho ya Yesu, na Gayo kwa kawaida alikuwa mfano bora wa kipekee wa huduma hii. Tunapaswa kufanya hivyo wakati wowote tunaweza, kukaribisha wamishenari wanaotutembelea, wahubiri na wageni (bora tu tuna uhakika kuwa ni waumini wa kweli) si tu kwa Makanisa yetu lakini pia kwa nyumba zetu, na kuwapa msaada wowote na faraja wanayohitaji.

Tunapaswa pia kuwa makini siku zote kufuata tu mfano wa wale ambao maneno na matendo yao yanaambatana Injili, na kuwa wafumbuzi wa kutosha kuweza kuwa na ufahamu wa wale kama vile Diotrefe ambaye tabia yake ni mbali na kuwa kama ile ambayo Yesu alifundisha.

English

Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kitabu cha 3 Yohana
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries