settings icon
share icon
Swali

Je! Mkristo anapaswa kutazamaje mazingira?

Jibu


Kuna tofauti kati ya mtazamo wa kibiblia wa mazingira na harakati ya kisiasa inayojulikana kama "mazingira." Kuelewa tofauti hii kutaunda maoni ya Mkristo kuhusu mazingira. Biblia ni wazi kwamba dunia na kila kitu kilicho ndani yake kilipewa na Mungu kwa mwanadamu kutawala juu yake na kudhibiti. "Mungu akawabarikia, Mungu akaawambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi"(Mwanzo 1:28). Kwa sababu waliumbwa kwa mfano Wake, Mungu aliwapa wanaume na wanawake nafasi ya pekee kati ya viumbe vyote na kuwaamuru wawe wasimamizi juu ya dunia (Mwanzo 1:26-28; Zaburi 8:6-8). Usimamizi unamaanisha kutunza, sio kutumia vibaya. Tunapaswa kusimamia kwa busara rasilimali ambazo Mungu ametupa, kwa kutumia jitihada zote za utunzaji kuzihifadhi na kuzilinda. Hii inaonekana katika Agano la Kale ambapo Mungu aliamuru mashamba na shamba ya mizabibu yatapandwa na kuvunwa kwa miaka sita, kisha kulimwa na kuachwa bila kupandwa mbegu kwa mwaka wa saba ili kujaza tena virutubishi vya udongo, yote mawili, kupumzisha ardhi na kuhakikisha kuendeleza utoaji kwa Watu wake katika siku zijazo (Kutoka 23:10-11; Mambo ya Walawi 25:1-7).

Mbali na jukumu letu la waangalizi, tunapaswa kufahamu utendaji na uzuri wa mazingira. Katika neema na nguvu Zake za ajabu, Mungu ameweka kila kitu juu ya sayari hii kinachohitajika kulisha, kuvaa, na nyumba mabilioni ya watu ambao wanaishi juu yake tangu Bustani ya Edeni. Rasilimali zote ambazo Yeye ametoa kwa mahitaji yetu zinatengenezwa upya, na Yeye anaendelea kutoa jua na mvua muhimu ili kuhimili na kujaza tena rasilimali hizo. Na kama hii haikuwa ya kutosha, Yeye pia ameipamba sayari kwa rangi za utukufu na mandhari nzuri kuvutia kwa hisia zetu za kupenda uzuri na kusisimua roho zetu kwa mshangao. Kuna aina nyingi za maua, ndege za kigeni, na maonyesho mengine ya kupendeza ya neema Yake kwetu.

Wakati huo huo, dunia tunayoishi si sayari ya kudumu, wala haikusudiwa kuwa. Harakati za mazingira zinateketezwa kwa kujaribu kuhifadhi sayari milele, na tunajua hii sio mpango wa Mungu. Anatuambia katika 2 Petro 3:10 kwamba mwishoni mwa umri, dunia na yote aliyoyaumba zitaharibiwa: "Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku huyo mbingu zitatoweka kwa mshondo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateteka". Dunia ya kimwili, ya kawaida katika hali yake ya sasa, pamoja na ulimwengu wote, itateketezwa na Mungu ataumba "mbingu mpya na dunia mpya" (2 Petro 3:13; Ufunuo 21:1).

Kwa hivyo tunaona kwamba badala ya kujaribu kuhifadhi dunia kwa maelfu au hata mamilioni ya miaka ijayo, tunapaswa kuwa wasimamizi wazuri wake almradi inadumu, ambayo itakuwa almradi inahudumia mpango huru na madhumuni ya Mungu.

English


Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Mkristo anapaswa kutazamaje mazingira?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries