settings icon
share icon
Swali

Kenosis ni nini?

Jibu


Neno "kenosis" linatokana na neno la Kiyunani kwa mafundisho ya kujitenga kwa Kristo katika mwili wake. The kenosis ilikuwa kujikana, si kujitenga mwenyewe wa uungu wala kubadilishana ya uungu kwa ubinadamu. Wafilipi 2: 7 inatuambia kwamba Yesu "bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu." Yesu hakuacha kuwa Mungu wakati wa huduma yake ya kidunia. Lakini aliweka kando utukufu wake wa mbinguni wa uhusiano wa uso kwa uso na Mungu. Pia aliweka kando mamlaka Yake ya kujitegemea. Wakati wa huduma yake duniani, Kristo alijitoa vikamilivu kwa mapenzi ya Baba.

Kama sehemu ya kenosis, wakati mwingine Yesu alifanya kazi na mapungufu ya ubinadamu (Yohana 4: 6, 19:28). Mungu hawezi kuchoka au kiu. Mathayo 24:36 inatuambia, "Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake." Tunaweza sitaajabu, kama Yesu alikuwa Mungu, atawezaje kukosa kujua kila kitu, kama Mungu anavyofanya (Zaburi 139: 1-6)? Inaonekana kwamba wakati Yesu alipokuwa duniani, alijitoa matumizi ya baadhi ya sifa zake za kimungu. Yesu bado alikuwa mtakatifu mkamilifu, mwenye haki, mwenye huruma, mwenye neema, mwenye ukweli, na mwenye upendo, lakini kwa viwango tofauti Yesu hakuwa mwenye ufahamu au mwenye nguvu.

Hata hivyo, linapokuja suala la kenosis, mara nyingi tunazingatia sana juu ya kile Yesu alitoa. Kenosis pia inahusika na kile Kristo alichochukua. Yesu alijiongezea Mwenyewe tabia ya kibinadamu na kujinyenyekeza Mwenyewe. Yesu alitoka kuwa utukufu wa utukufu mbinguni kuwa mwanadamu aliyeuliwa msalabani. Wafilipi 2: 7-8 inasema, "bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu: tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii ata mauti, naam, — mauti ya msalaba." Katika kitendo cha mwisho cha unyenyekevu, Mungu wa ulimwengu alikuja kuwa mwanadamu na alikufa kwa ajili ya uumbaji Wake. Kwa hiyo, kenosis ni Kristo anayezingatia hali ya kibinadamu na upungufu wake wote, isipokuwa bila dhambi.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kenosis ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries