settings icon
share icon
Swali

Ni hatua gani kuelekea wokovu?

Jibu


Watu wengi wanatafuta “hatua kuelekea wokovu.” Watu wanapenda dhana ya kitabu cha mwongozo wa hatua tano, kwamba ikiwa sitafuatwa, zitaelekeza wokovuni. Mfano wa haya ni Waislamu na nguzo zao tano. Kulingana na Waislamu, ikiwa nguzo hizo tano zimefuatwa wokovu utapatikana. Kwa sababu ya dhana ya mchakato wa hatua kwa hatua kwa wokovu ni wa kusihi, wengi wa Wakristo katika jamii wanawazilisha wokovu kuwa kama ni ule upatikanao kwa ajili ya kufuata mchakato wa hatua kwa hatua. Kinisa la Kikatholiki la Kirumi liko na sakaramenti saba. Madhehebu mbali mbali la Wakristo wanaongeza ubatizo, kutubu hadharani, kugeuka kutoka dhabi na kuongea katika ndimi na kadhalika, kama hatua za wokovu. Lakini Biblia yawazilisha hatua moja ya wokovu. Wakati mfilipi mfungwa alimwuliza Paulo, “Nitafanya nini ili niokoke?” Paulo alimjibu, “Mwamini Bwana Yesu na utaokolewa” (Matendo 16:30-31)

Imani katika Yesu kama mwokozi ndio “hatua” pekee ya wokovu. Ujumbe wa Biblia uu wazi. Wote tumetenda dhambi kinyume na Mungu (Warumi 3:23). Kwa sababu ya dhambi zetu, tunastahili kutenganishwa na Mungu milele (Warumi 6:23). Kwa sababu ya upendo wake kwetu (Yohana 3:16), Mungu aliuchukua umbo la mwanadamu na akafa kwa ajili yetu, huku akichukua adhabu ambayo tulistahili (Warumi 5:8; 2Wakorintho 5:21). Mungu anaahidi msamaha wa dhambi na uzima wa milele mbinguni kwa wote wampokeao, kwa neema kupitia kwa imani katika Yesu Kristo kwa mwokozi (Yohana 1:12; 3:16; 5:24; Matendo 16:31).

Wokovu sio juu ya hatua fulani ambazo ni lazima tuzifuate ile tupate wokovu. Naam, Wakristo lazima wabatizwe. Naam, Wakristo lazima wamkiri hadharani Kristo ni mwokozi. Naam Wakristo lazima wageuke kutoka dhambi. Naam, Wakristo lazima wayatoe maisha yao kwa kumtii Mungu. Ingawa, hizi sio hatua za wokovu. Ni matokeo ya wokovu. Kwa sababu ya dhambi zetu, kwa njia yoyote hatuwezi jipatia wokovu. Tunaweza fuata hatua 1000, na hazitatosha. Ndio sababu Yesu akafa kwa ajili yetu. Kamwe hatuna uwezo wa kulipia dhambi zetu kwa Mungu kama deni ili tujitakaze kutoka dhambi. Ni mungu pekee angekamilisha wokovu, na kwa hivyo alifanya. Mungu mwenyewe alikamilisha “hatua” na papo hapo akautoa wokovu kwa ye yote atakayeupokea kutoka kwake.

Wokovu na msamaha wa dhambi sio mambo na hatua. Ni kumpokea Kristo kama mwokozi na kutambua ya kwamba amekwisha fanya kazi yote kwa niapa yetu. Mungu anahitaji hatua moja kutoka kwetu-kumpokea Yesu Kristo kama mwokozi na kumwamini Yeye pekee kama njia ya wokovu. Hiyo ndio yatofautisha imani ya Kikristo kutoka kwa dini zote za ulimwengu, ambazo kila moja iko na orodha ya hatua ambazo ni lazima zifuatwe ili wokovu upatikane. Imani ya Kikristo yatambua ya kwamba Mungu amekwisha kamilisha hatua, na anatuita tumpokee kwa imani.

Je, umefanya uamuzi kwa Kristo kwa kile ulicho soma hapa? kama ndiyo, tafadhali bonyeza kwa “Nime mkubali Kristo hivi leo” hapo chini.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni hatua gani kuelekea wokovu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries