settings icon
share icon
Swali

Je! Wakristo wanastahili kwenda kwa madaktari?

Jibu


Kunao Wakristo wengine wanaoamini kuwa kutafuta msaada wa madaktari kunaonyehsa kutokuwa na imani kwa Mungu. Katika kikundi Neno-Imani, kumwona daktari kila mara inachukuliwa kuwa kutokuwa na imani ambayo itamzuia Mungu kukuponya. Kwa makundi kama, Wakristo Wasayansi, wanaotafuta usaidizi wa matibabu wakati mwingine unatazamwa kuwa kizuizi cha kutumia nguvu zetu za kiroho ambazo Mungu ametupa kujitibu. Utata wa mtazamo huu hasa umekosa. Ikiwa gari yako imearibiwa, unaipeleka kwa makanika au unangoja Mungu kutenda muujiza na kutengeza gari yako? Kama mfereji wa kupitishia maji kwa nyumba yako umetoboka, unamngoja Mungu kuunda mahali unadondoa maji, au unamwita fundi? Mungu ako na uwezo wa kuiunda gari yako au kukarabati mfereji vile anavyofanya uponyaji katika miili yetu. Hoja kwamba Mungu anaweza na anatenda miujiza ya uponyaji haimanishi kuwa kila mara tutarajie muujiza badala ya kutafuta msaada kutoka kwa mtu aliye na ujuzi na maarifa ya kutuzaidia.

Madaktari kwetu tumeelezwa takribani dazeni katika Bibilia. Aya peke ambayo inaweza kuchukuliwa kuwa nche ya muktadha kwa kufunza ambayo mtu hastahili kwenda kwa daktari itakuwa 2 Mambo Ya Nyakati 16:12. “Akashikwa Asa na ugonjwa wa miguu katika mwaka wa thelathini na kenda wa kumiliki kwake; ugonjwa wake ukazidi sana; lakini hakumtafuta BWANA katika ugonjwa wake, bali waganga.” Shida haikuwa kuwa Asa aliwatafuta waganga, lakini kuwa “hakumtafuta BWANA.” Hata wakati unamtembelea daktari, upeo wa imani yetu uwe kwa Mungu si kwa daktari.

Kunayo aya nyingi ambazo zazungumzia kutumia “madawa ya matibabu” kama vile kuweka viziba donda (Isaya 1:6), mafuta (Yakobo 5:14), mafuta na divai (Luka 10: 34), majani (Ezekieli 47: 12), divai (1 Timotheo 5: 23), na marhamu, hasa “zeri ya Gileadi” (Yeremia 8:22). Pia Luka mwandishi wa Matendo Ya Mitume na injili ya Luka tunaambiwa kuwa na Paulo yeye ni “tabibu mpendwa” (Wakolosai 4:14).

Mariko 5: 25-30 yahusiana na hadhiti ya mwanamke aliye kuwa na shida ya uvujaji damu, shida ambayo matabibu hawangeweza kuitibu ingawa alikuwa amewatembelea madaktari wengi na akatumia pesa zake zote alizokuwa nazo. Kukuja kwa Yesu, alifikiria kuwa akiguza pindo la nguo yake atapona; akaguza pindo la nguo yake na akaponywa. Yesu kwa kuwajibu Mafarisayo ya kuwa ni kwa nini alichukua muda wake mwingi na wenye dhambi aliwaambia, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi” (Mathayo 9:12). Kutoka kwa aya hii mtu anaweza kusonga kutoka kwa kanuni hizi:

1) Matabibu si Mungu na wazitazamiwe kuwa Mungu. Wakati mwingine wanweza kuzaidia, lakini kutakuwa na wakati mwingine ambao watakayo yafikia ni kuchukua pesa zako.

2) Kumuona tabibu na kutumia njia za “kunduia” zimelaaniwa katika maandiko. Kwa kweli matibabu yanachukuliwa kuwa mazuri sana

3) Katika upungu wo wote wa nje wa mwili lazima tutafute Mungu kuingilia kati (Yakobo 4:2; 5:13). Mungu ahaidi kuwa atajibu sawa na vile tatakavyo hitaji kila wakati (Isaya 55: 8-9), lakini tuko na uakikisho kuwa yote ayafanyayo yatafanywa kwa upendo na kwa hivyo kwa manufaa yetu (Zaburi 145: 8-9).

Kwa hivyo, Wakristo wanastahili kwenda kwa madaktari? Mungu alituumba viumbe werevu na kutupa uwezo kuunda madawa na kujifunza jinsi ya kutibu miili yetu. Hakuna ubaya wo wote kwa kutumia ujuzi huu na uwzo kwa kutibu. Matabibu wanaweza kuonwa kama kipaji cha Mungu kwetu, njia ambayo kwayo Mungu analeta uponyaji. Kwa wakati huo huo, imani yetu inastahili kuwa kwa Mungu, si kwa madaktari au madawa. Kwa maamuzi yote magumu, tumtafute Mungu aliyeahidi kutupa hekima wakati tunaiuliza (Yakobo 1: 5).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Wakristo wanastahili kwenda kwa madaktari?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries