settings icon
share icon
Swali

Nitawezaje kosa kuenda jahannam?

Jibu


Kutoenda jehannam ni rahisi na vile unavyo dhani. Watu wengine wanaamini kuwa lazima watii amri kumi katika maisha yao yote ili wasiende jahannam. Watu wengine wanafikiria ni lazima watunze tamaduni fulani ili wasiende jahannam. Na watu wengine wanaamini kuwa hakuna uwezekano wa kujua hakika hutaenda jahannam. Kati ya mitazamo hii hakuna hata moja ni sawa. Biblia ii wazi jinzi ya mtu anavyo epuka kwenda jehannam baada ya kifo.

Biblia yaelezea wazi jahannam kuwa ni mahali pa kustaajabiza. Jahannam inaelezewa kama mahali pa “moto wa milele” (Mathayo 25:41), “Moto usiozimika” (Mathayo 3:12), “Mahali pa aibu na kusaga meno” (Daniel 12:2), mahali ampapo “moto hauzimiki” (Marko 9:44-49), na “uaribivu kwa milele” (2Wathesalonike 1:9). Ufunuo 20:10 yaelezea jahannam kama “siwa la moto uchomao” mahali wenye dhambi “watachomwa mchana na usiku milele yete (Ufunuo 20:10). Bila kupinga jahannam ni mahali tunastahili kuepuka.

Ni kwa nini jahannam ipo na ni kwa nini Mungu awatume watu wengine huko? Biblia inatuambia ya kwamba Mungu ”aliiandaa” jahannam kwa Ibilisi na malaika walioanguka baada ya kumuasi Mungu (Mathayo 25:41). Wale walio kataa kipaji cha Mungu cha msamaha watatezeka njia hiyo hiyo ya Ibilisi na malaika walio asi. Ni kwa nini jahannam ni ya maana? Dhambi zote zi kinyume na Mungu (Zaburi 51:4), na jinsi Mungu anaishi milele, hukumu ya milele ndio inayo faa. Jahannam ni mahali ambapo haki ya utakatifu ya Mungu inatendeka. Jahannam ni mahali ambapo Mungu anaihukumu dhambi na wale wote walio mkataa. Biblia yaiweka wazi kwamba wote tumetenda dhambi (Mhubiri 7:20; Warumi 3:10-23), kwa mjibu wa hayo, wote tunastahili kwendwa jahannam.

Sasa, tunawezaje kuepuka jahannam? Jinsi hukumu ya milele ndiyo inayofaa, fidia ya milele na isiyo haribika lazima ilipwe. Mungu akawa mwanadamu katika mwili wa Yesu Kristo. Katika Kristo Yesu, Mungu aliishi nasi, akatufunza, na akatuponya- mambo hayo hayakuwa lengo lake la mwisho. Mungu akawa mwanadamu (Yohana 1:1,14) ili aweze kufa kwa ajili yetu. Yesu ambaye ni Mungu katika mwili wa mwanadamu alikufa msalabani. Kama Mungu, kifo chake kikawa na dhamani isiyo na mwisho, na kikalipa deni yote ya dhambi (1Yohana 2:2). Mungu anatualika tumpokee Yesu Kristo kama mwokozi, kwa kukubali kifo chake kama fidia kamili ya dhambi zetu. Mungu anaahidi ya kwamba ye yote atakayemwamini Yesu (Yohana 3:16), kumtuma inia yeye peke kama mwokozi (Yohana 14:6), ataokolewa kwa mfano, haendi jahannam.

Mungu hapendi mtu ye yote aende jahannam (2Peter 3:9). Ndio sababu Mungu alifanya dhabihu kamili na yenye inatosha kwa niapa yetu. Kama hutaki kwenda jahannam mpokee Yesu kama mwokozi wa maisha yako. Hiyo iko rahisi hivyo tu. Mwambie Mungu kwamba umetambua wewe ni mwenye dhambi na unastahili kwenda jahannam. Mwambie Mungu ya kwamba unamwamini Yesu Kristo kama mwokozi wako. Mshukuru Mungu kwa kuutoa wokovu na ukombozi kutoka jahannam. Imani rahisi ni kumwani Yesu Kristo kama mwokozi, ndio njia unaweza kuepuka kwenda jahannam!

Je, umefanya uamuzi kwa Kristo kwa kile ulicho soma hapa? kama ndiyo, tafadhali bonyeza kwa “Nime mkubali Kristo hivi leo” hapo chini.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nitawezaje kosa kuenda jahannam?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries