settings icon
share icon
Swali

Niko katika harakati za kupata talaka. Je! Ninaweza kuanza kuchumbiana, au nisubiri hadi talaka ifanyike?

Jibu


Swali la kuchumbiana wakati wa mchakato wa talaka ni gumu kulijibu kwa sababu kadhaa. Kwanza, dhana ya “kuchumbiana” kama tunavyoijua hii leo haijatajwa popote katika Biblia. Ndoa nyingi katika nyakati za Biblia zilipangwa, na mawasiliano yoyote kati ya wale waliotazamiwa kuwa wenzi wa ndoa yalidhibitiwa kabisa. Kwa kuongezea, haijalishi yeyote ana maoni gani kuhusu suala la talaka, ni muhimu kukumbuka Malaki 2:16: “Ninachukia kuachana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli.” Kulingana na Biblia, ndoa ni ahadi ya maisha yote. “Hivyo si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe” (Mathayo 19:6). Hakuna uamuzi wa talaka unapaswa kufanywa kirahisi.

Kunazo hali tatu ambazo kuchumbiana wakati wa machakato wa talaka kunaweza kutokea. Ya kwanza ni hali ya mwenzi ambaye ana sababu za kibiblia za talaka. Yaani yule mwenzi asiye na hatia ameachwa na mwenzi wake asiyeamini au ametapeliwa na mzinzi asiyetubu. Vyovyote vile, mwenzi asiye na hatia anaweza kuwa katika hali ya msukosuko wa kihisia-moyo na udhaifu. Watu wengi walio katika mchakato wa talaka, hata kama si kosa lao na hata wakati wana sababu za kibiblia, kwa kawaida huvunjika moyo na hawako katika hali nzuri kiakili ya “kuchumbiana.” Kwa kawaida watu hawafanyi maamuzi mazuri wakiwa katika hali ya “msukosuko kwa sababu ya uhusiano uliovunjika.” Kwa mtu aliyetalikiwa na bado anaumia au mtu aliye katika mchakato wa talaka ya uchungu, kuanza uchumba sio jambo la busara au hekima. Mwenzi aliyeachwa kwa kweli anaweza kuwa mpweke lakini kufanya maamuzi ya uhusiano wa kimungu yaliyo waziwazi katika hali kama hiyo ni vigumu, au haiwezekani.

Hali ya pili ambayo uchumba wakati wa mchakato wa talaka unaweza kutokea ni ile ya mtu anayemtaliki mwenzi wake kwa sababu zisizo za Kibiblia. Talaka katika kesi hii, kwa meneno yake Mungu, inatokana na “ugumu wa moyo” (Marko 10:1-12). Kwa hivyo, talaka kama hiyo, ni upungufu wa kiroho na inapaswa kuwasukuma wale wanaohusika kumtazamia Bwana na si kutafuta kujaza pengo la yule wanayemtaliki.

Hali ya tatu ambayo kuchumbiana wakati wa mchakato wa talaka kunaweza kutokea ni ile ya mtu ambaye husababisha talaka, yaani, mtu mwenye hatia” katika talaka. Nafasi zote za kibiblia za kuoa tena baada ya talaka zinahusiana na mwenzi “asiye na hatia” katika talaka yenye misingi ya kibiblia. Hakuna kibali cha kibiblia cha kuoa tena kwa mwenzi aliyetalikiana kwa sababu zisizo za kibiblia au kwa mwenzi aliyesababisha talaka, iwe kwa uzinzi, kuachwa, na/au sababu zinginezo. Biblia haisemi popote kwamba mwenzi “mwenye hatia” katika talaka anaruhusiwa kuoa tena; kwa hiyo, hapaswi kuchumbiana.

Kwa kuwa kusudi la kuchumbiana ili kutafuta mwenzi wa ndoa au kutafuta urafiki na watu wa jinsia tafauti, kulingana na Biblia mwanamume au mwanamke aliyeolewa hayuko huru kuchumbiana, hata ikiwa kuna talaka inayosubiri. Hata mhasiriwa asiye na hatia wa talaka ambayo haitaki bado yuko kwenye ndoa hadi ndoa itakapokomeshwa kisheria au rasmi. Kuanzisha uhusiano wa uchumba nje ya ndoa, hata kwa wale wanaopata talaka, hutoa mtazamo mbaya. Chaguo bora zaidi ni kujiepusha na tendo lolote linaloweza kuhatarisha mtu kiroho au kutoa mtazamo kwa wengine kwamba mtu fulani haijali ndoa.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Niko katika harakati za kupata talaka. Je! Ninaweza kuanza kuchumbiana, au nisubiri hadi talaka ifanyike?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries