settings icon
share icon
Swali

Je! Kutakuwa na ngono mbinguni?

Jibu


Biblia haizungumzii mada ya ngono mbinguni. Bila maelezo ya wazi katika Maandiko juu ya suala hili, hatuwezi kusema “naam” au “la” kuhusu uwezekano wa ngono mbinguni. Hata hivyo, Biblia inazungumzia jambo linalohusiana na hilo; ndoa mbingu au, kwa usahihi zaidi, ndoa baada ya ufufuo

Katika Mathayo 22 Masadukayo wanajribu kumvunjia heshima Yesu kwa kuuliza swali waliloliona kuwa gumu kuhusu ndoa na ufufuo. Walikuja Kwake na kuwasilisha kesi ya dhahania ambapo mwanamke alikuwa ameolewa mara nyingi maishani mwake. Kisha wakauliza ni mume gani angekuwa wake katika ufufuo: “Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?” (aya ya 28). Yesu aliwajibu kwa maneno haya: “Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.” (aya ya 30).

Ukweli kwamba hakuna kuoa mbinguni unaonyesha kwamba hakuna ngono mbinguni, ingawa Bwana hafikii haitimishi hilo kwa wazi. Mafundisho ya wazi ya Yesu katika Mathayo 22:29-32 ni 1) ufufuo utafanyika na 2) ndoa haitakuwa tena sehemu ya uzoefu wetu. Inaonekana kwamba ndoa ni uhusiano wa kufurahia katika maisha haya, lakini hautasonga mbele katika maisha yajayo. Hatupotezi utambulisho wetu mbinguni (ona Luka 16:23), lakini hatutashikilia mahusiano sawa tunayofanya duniani. Kuwepo kwetu kutakuwa tofauti kabisa na vile tulivyozoea hapa ulimwenguni.

Kutokana na ukweli kwamba mbinguni hakuna ndoa tunakisia angalau mambo mengine mawili:

1) Hakutakuwa na uzazi mbingini. Idadi ya waliokombolewa imewekwa, na, bila kifo, hakutakuwa na haja ya kuendeleza jamii ya wanadamu

2) Hakutakuwa na kujamiiana mbinguni. Tamaa na matamanio ya ulimwengu huu yatatoa nafasi kwa furaha ya juu na yenye kuridhisha zaidi katika ulimwengu ujao.

Hakutakuwa na haja ya kufanya ngono mbinguni, kama vile kutakuwa hakuna haja ya mambo mengine mengi. Kwa karne nyingi, hekalu la Yerusalemu na dhabihu zilizotolewa huko zilikuwa kitovu cha ibada, lakini, mara Kristo alipojitoa Mwenyewe kama dhabihu ya mwisho hekalu na mfumo wa dhabihu haukuhitajika tena (Yohana 4:22-23). Walikuwa “nakala za mambo ya mbinguni” (Waebrania 9:23). Kwa njia hiyo hiyo, uhusiano wa ndoa na picha ya uhisano wetu na Kristo (Waefeso 5:31-32). Tutakapokuwa pamoja na Kristo, mfano huo hautahitajika tena. Tutakuwa na ukweli, ambao ni bora zaidi kuliko uwakilishi wowote wa kidunia. Hii ndiyo sababu Yesu anaitwa Bwana-arusi, Kanisa linaitwa Bibi-arusi Wake, na sherehe yetu mbinguni inatiwa Karamu (Yohana 3:29; Mathayo 22:1-14; Ufunuo 19:7-9).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Kutakuwa na ngono mbinguni?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries