settings icon
share icon
Swali

Je, Biblia inaunga mkono ndoa za kupangwa?

Jibu


Ndoa “iliyopangwa” ni ile ambayo imeridhiwa na wazazi na wazazi wa bibi na bwana harusi, na mara nyingi bila kuzingatia matakwa ya wanandoa watakaofunga ndoa. Biblia haisemi kwamba wazazi wanapaswa kupanga ndoa, wala haisemi kwamba hawapaswi kupanga ndoa. Hata hivyo, kuna ndoa chache zilizopangwa katika Biblia, hasa ndoa ya Isaka na Rebeka.

Katika simulizi hio, mtumishi aliyeaminika alitumwa na babake Isaka, Abrahamu, kutafuta mchumba anayefaa kutoka kwa watu wa ukoo wake kwa sababu hakutaka Isaka kuoa bibi kutoka kwa Wakanaani wapagani (Mwanzo 24). Tunaona kutokana na majibu ya Rebeka kuwa alikuwa na sifa nyingi za kimungu, alikuwa chaguo la Mungu kwa Isaka. Kwa hakika, sio ndoa zote zilizopangwa wakati huo zifanywa katika njia hiyo ya kimungu nay a utii.

Desturi ya ndoa za kupanga iliendelezwa katika tamaduni nyingi, ikiwa ni pamoja na tamaguni za Magharibi, hadi miaka ya 1900. Hata leo, katika familia za haliza za Kiyahudi, Kiislamu, kihindu, ndoa za kupangwa zinafanyika. Biblia iko kimya juu ya swala hili. Hata hivyo, Biblia inaeleza jinsi mwenzi wa kiungu anapaswa kuwa. Kwa Mkristo, ndoa iwe imepangwa au la, inapaswa kufanywa kwa mtu mwingine katika imani. Uhusiano muhimu ambao kila mmoja wetu anao ni uhusiano wet una Bwana Yesu Kristo. Mwenzi tunaye mchagua anapaswa kuwa ambaye ana lengo la kutembea kwa utii wa Neno la Mungu na anayeazimia kuishi ili maisha yake yamletee Mungu utukufu (1 Wakorintho 10:31).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, Biblia inaunga mkono ndoa za kupangwa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries