settings icon
share icon
Swali

Je! Umomoni ni dhehebu? Wamomoni wanaamini nini?

Jibu


Dini ya Kimomoni, ambayo wafuasi wake wanajulikana kama Wamomoni na Latter Day Saints (LSD), ilianzishwa chini ya miaka miambili iliyopita na mtu anayeitwa Joseph Smith. Alisema kwamba alitembelewa na Mungu Baba na Yesu Kristo ambaye alimwambia kwamba Makanisa yote na kanunu zao za imani zilikuwa chukizo kwake. Joseph Smith akatoka na kuanzisha dini nyigine ambayo ilidai kuwa “ndio kanisa ya kweli duniani.” Kasoro na Wamomoni ni kwamba inachanganyisha, inarembesha, na kupanua juu ya Bibilia. Wakristo hawana sababu yo yote ya kuamini kuwa Bibilia si kweli na kamili. Kumwamini Mungu kwa kweli yamaanisha kuwa unaamini katika neno lake, na maandiko yote ni pumzi ya Mungu, ambayo yamaanisha yalitoka kwake (Timotheo 3:16).

Wamomoni wanaamini kuwa kunayo sehemu nne za pumzi kiungu za neno sio moja tu peke: 1) Bibilia “vile imefasirwa vizuri sana.” Ni aya gani ambazo zinachukuliwa kuwa si kweli kila wakati haziwekwi wazi. 2) Kitabu cha Wamomoni, ambacho “kilifasiriwa” na Smith na kuchapishwa mwaka wa 1980. Smith alidai ndicho “kitabu peke cha kweli.” 3) Kanuni na maagano, ambayo kilikuwa na mkusanyiko wa ufunuo wa siku hizi kuhusu “Kanisa la Yesu Kristo vile limerejeshwa.” 4) Lulu ya dhami sana, ambayo inachukuliwa na Wamomoni “kufafanua” kanuni na mafunzo ambayo yalipotezwa kutoka kwa Bibilia na kuongezea .ujumbe ulio wake kuhusu uumbaji wa dunia.

Momoni wanaamini yafuatayo kuhusu Mungu: Hakuwa kiumbe cha mamlaka ya juu sana juu ya ulimwengu, lakini alipokea mamlaka hayo kupitia kwa kuishi maisha takatifu na bidii yake isiyo na mwisho. Wanaamini kuwa Mungu Baba ako na “mwili wa nyama na mifupa inaguzika kama ya mwanadamu.” Ingawa alitengwa na viongozi wa siku hizi wa Momoni, Brigham Young alifunza kuwa Adamu awali alikuwa Mungu na baba wa Yesu Kristo. Kwa ulinganisho, Wakristo wanajua haya kuhusu Mungu: kunaye Mungu mmoja wa kweli (Kumbukumbu La Torati 6:4; Isaya 43:10; 44:6-8), amekuwa akiishi na atakuwa akiishi (Kumbukumbu La Torati 33:27; Zaburi 90:2; 1 Timotheo 1:17), na hakuumbwa bali yeye ndiye alikuwa muumbaji (Mwanzo 1; Zaburi 24:1; Isaya 37:16). Yeye ni mkamilifu na hakuna mwingine amfananaye (Zaburi 15:29; Hosea 11:9). Yeye ni Roho (Yohana 4:24), na Roho haitengenezwi kwa nyama na mifupa.

Momoni wanaamini kuwa kuna viwango tofauti au falme tofauti katika maisha baada ya kifo: ufalme wa peponi, ufalme wa duniani, na giza la nche. Mahali ambao mwanadamu atamalizia kutegemea chenye wanaamini na kufanya katika maisha haya. Kwa ulinganisho, Bibilia inatuambia baada ya kifo, tunaenda mbinguni au jahannamu kulingana na kama tulikuwa au hatukuwa na imani katika Yesu Kristo kama Bwana na mwokozi wetu. Kutoweka kutoka kwa mwili wetu yamaanisha, sisi kama waumini, tuko na Mungu (2 Wokorintho 5:6-8). Wasio amini watatumwa jahannamu au mahali pa wafu (Luka 15:50-54). Kutakuwa na mbingu mpya na nchi mpya kwa waumini (Ufunuo 21:1) na wasio amini watatupwa katika zila la moto (Ufunuo 20:11-15). Hakuna nafasi ya pili ukombozi baada ya kifo (Waebrania 9:27).

Viongozi wa Momoni wamefunza kuwa ubadilisho wa Yesu ulitokea kwa minajili ya ule uhisiano wa kimwili wa Mungu Baba na Mariamu. Wamomoni wanaamini kuwa Yesu ni mungu , lakini binadamu yeyote anaweza kuwa mungu. Momoni wanafunza kwamba wokovu unaweza patikana kwa kuweka pamoja imani na matendo mazuri. Kinyume na hii, Wakristo katika historia wamekuwa wakifunza hakuna mtu atakaye fikia cheo cha Mungu- ni yeye peke ambaye ni mtakatifu (1 Samueli 2:2). Tunaweza fanywa watakatifu mbele za Mungu kupitia kwa imani kwake (1 Wakorintho 1:2). Yesu ndiye Mwana wa peke wa Mungu (Yohana 3:16), yeye ndiye peke ambaye amewai ishi bila dhambi, maisha yasiyo na mawaa, na sasa ako na heshima ya juu sana mbinguni (Waebrania 7:26). Yesu na Mungu wote ni kitu kimoja, Yesu kuwa ndiye peke aliishi baada ya kuzaliwa kimwili (Yohana 1:1-8; 8:56). Yesu alijotoa yeye mwenye kama dhabihu kwetu, Mugu akamfufua kutoka kwa kaburi, na siku moja kila mmoja atalikiri kuwa Kristo ni Bwana (Wafilipi 2:6-11). Yesu anatuambia ni vigumu kuingia mbinguni kwa matendo yetu na kwamba ni kwa imani peke ndani yake itawezekana (Mathayo 19:26). Wote tunastahali hukumu ya milele kwa sababu ya dhambi zetu, lakini Mungu kwa upendo wake usio na mwisho na neema vimetuwezeshea njia. “Kwa maana wote mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu” (Warumi 6:23).

Hakika kunayo njia moja peke ya kupata wokovu na ni kumjua Mungu na Mwanawe, Yesu (Yohana 17:3). Wokovu haupatikani kwa matendo, bali kwa imani (Warumi 1:17; 3:28). Tutaipokea zawadi hii, haijalishi sisi ni nani au ni nini tumefanya (Warumi 3:22). “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolwea kwalo” (Matendo Ya Mitume 4:12).

Ingwa Wamomoni ni watu wa urafiki, wa upendo, na ni watu wakarimu, wamedanganywa na dini za uongo ambazo zageuza hali ya Mungu, utu wa Yesu Kriso, na njia za wokovu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Umomoni ni dhehebu? Wamomoni wanaamini nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries