settings icon
share icon
Swali

Je! inaruhusiwa kwa Mkristo kuwa na mwenzi wa maisha bila ndoa ya kiserikali?

Jibu


Kunayo mambo kadhaa ya kuzingatia katika swali hili. Kwanza kabisa, hebu tufafanue “Mkristo.” Watu wengi hufikiri wao ni Wakristo kwa sababu hawajihusishi na dini yoyote. Wanaenda kanisani na kukubaliana na mengi ya yale ambayo Biblia inasema. Hata hivyo, Biblia inafafanua Mkristo kuwa mwanafunzi au mfuasi, wa Bwana Yesu Kristo (Matendo 11:26). Mkristo ni mtu ambaye amekubali kifo, kuzikwa, na ufufuo wa Bwana Yesu Kristo kama malipo ya dhambi yake mwenyewe (Yohana 1:12; Matendo 16:31). Mwanafunzi wa Kristo amechagua “kujikana mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, amfuate” Yesu (Luka 9:23). Kwa hiyo, chochote Yesu anachosema tufanye kupitia Neno Lake, Mkristo anapaswa kufanya. Hatuwi Wakristo kwa kufanya mambo mema; lakini, kwa sababu sisi ni Wakristo, tunataka kumtii Yesu katika mambo yote (Waefeso 2:8-9; Yakobo 2:26). Katika Yohana 15:14, Yesu alisema, “Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.”

Kwa hiyo Mkristo hufanya uchaguzi wa maisha kulingana na kile kinachomtukuza Yesu (1 Wakorintho 10:31). Kuliko kuuliza kama hali “inaruhusiwa” afadhali kuuliza “Hii itamtukuza Bwana wangu namna gani?” Mungu alianzisha ndoa, na ni ufafanuzi wake tunapaswa kuutumia kama msingi wetu. Mungu anafafanua ndoa kuwa uhusiano wa kudumu ambapo mwanamume huwaacha baba na mama yake na kuungana na mke. Wote wawili wanakua “mwili mmoja,” na muunganiko huo hapaswi kutenganishwa na mapenzi ya mwanadamu (Mwanza 2:24; Marko 10:7-9; Waefeso 5:31). Malaki 2:14 inatuambia kwamba sababu moja ni kwa nini Mungu anachukia talaka ni kwamba Yeye alikuwa pale wakati wanandoa walichukua nathiri zao. Kibiblia, ndoa ni muunganiko wa kiagano wa mume na mke katika kiroho na kimwili katika maisha yao yote. Muunganiko huo ndio sababu ya kusherekea na unastahili heshima yetu.

Baadhi ya wanandoa hii leo, hasa miongoni mwa wazee, wanataka kuishi pamoja kama wanandoa “waliooana” bila kuoana kisheria. Mara nyingi hii inafanywa kwa manufaa fulani ya kifedha au hisia ya kutaka kuifanya rahisi. Baadhi ya wanandoa hawa hufanya sherehe za kidini kanisani na hujiona kuwa wamefunga ndoa mbele za Mungu. Hata hivyo, wanandoa wanaotafuta “ndoa ya kiroho” huku wakiepuka ndoa halali wanatafuta kukwepa matakwa ya sheria, na hiyo inaleta matatizo mapya kwa Mkristo (Warumi 13:1-7). Ikiwa wanandoa wakubwa (kwa umri) wanaamini kuwa ni mapenzi ya Mungu wawe pamoja, wanapaswa kufunga ndoa kwa mujibu wa sheria za nchi, na kumtumainia Mungu kwa ajili ya fedha.

Hakuna msingi wowote wa kimaandiko wa hali ya kuishi pamoja, hata kama wapenzi hao wawili wanaohusika wanakusudia kuwa mume na mke mmoja maishani. Nia hujaribiwa, na ukosefu wa ahadi ya kweli ya ndoa hufanya iwe rahisi kutengana. Bila ndoa, uhusiano huo ni wa usherati na unashutumiwa katika Maandiko (Wagalatia 5:19; Waefeso 5:3; 1 Wathesalonike 4:2). Neno “mwenzi wa maisha” ni la kutilia shaka sauti na lenye historia yenye shaka. Ina maana kwamba uhusiano huo haujaidhinishwa kisheria au kimaadili na kwamba huenda usidumu. Inaepuka agano ambalo Mungu aliunda kwa ajili ya ndoa. Kwa wenzi wa ndoa Wakristo, neno kama hilo linaweza kutia shaka mara moja sifa yao na, hatimaye juu ya sifa ya Kristo. Wenzi wowote wa ndoa Wakristo wanaofikiria “ushirika wa maisha” wanapaswa kuuliza, “Je! kupuuza kwetu kwa ndoa ya kitamaduni kutamtukuzaje Bwana Yesu?”

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! inaruhusiwa kwa Mkristo kuwa na mwenzi wa maisha bila ndoa ya kiserikali?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries