settings icon
share icon
Swali

Mihuri saba na tarumbeta saba katika kitabu cha Ufunuo ni nini?

Jibu


Mihuri saba (Ufunuo 6:1-17, 8:1-5 tarumbeta saba (Ufunuo 8:6-21, 11:15-19), na mabakuli saba (Ufunuo 16:1-21) ni msuluro wa aina tatu za hukumu nyakati za mwisho hukumu kutoka kwa Mungu. Hukumu itaendelea kuwa mbaya zaidi nay a kustaajabisha pakubwa huku nyakati za mwisho sikiendelea. Mihuri saba, tarumbeta, na bakuli ni kushikamana zimeunganishwa. Mhuri wa saba utakaribisha tarumbeta saba (Ufunuo 8:1-5), na baragumu ya saba itakaribisha bakuli saba (Ufunuo 11:15-19, 15:1-8).

za kwanza nne kati ya ile mihuri saba zinajulikana kama farasi wanne wa ufunuo. Muhuri wa kwanza unakaribisha Mpinga Kristo (Ufunuo 6:12). Mhuri wa pili husababisha vita vikubwa (Ufunuo 6:3-4). Tatu wa ile mihuri saba husababisha njaa (Ufunuo 6:5-6). Mhuri wa nne utaleta pigo la njaa zaidi, na vita zaidi (Ufunuo 6:7-8).

Mhuri wa tano inatuambia kuhusu wale ambao watakuwa mashahidi kwa ajili ya imani yao katika Kristo nyakati za mwisho (Ufunuo 6:9-11). Mungu anasikia kilio chao kwa ajili ya haki na kutoa katika muda wake katika mfano wa muhuri wa sita, pamoja na tarumbeta na bakuli ya hukumu. Wakati mhuri wa sita kati ya ile mihuri saba utatokea, tetemeko la ardhi hutokea, na kusababisha mageuzi mkubwa na ya kutisha na uharibifu -pamoja na matukio ya angani kawaida (Ufunuo 6:12-14). Wale ambao wanaishi wana haki ya kupiga kelele, "Tuangukieni, tusitirini mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi na hasira ya mwana kondoo. Kwa maana siku kuu, ya hasira yao, imekuja, na yeye ni nani awezaye kusimama?" (Ufunuo 6:16-17).

Tarumbeta saba zimeelezewa katika Ufunuo 8:6-21. Tarumbeta saba ni yale "yaliyomo" katika mhuri wa saba (Ufunuo 8:1-5). Baragumu ya kwanza husababisha mvua ya theluji na moto ambao utaiharibu mimea katika dunia (Ufunuo 8:7). Mbiu ya pili huleta kile kinaonekana kuwa mlima kupiga bahari na kusababisha kifo cha viumbe vya baharini (Ufunuo 8:8-9). Mbiu ya tatu ni sawa na ya pili, ila unaathiri maziwa duniani na mito badala ya bahari (Ufunuo 8:10-11).

Tarumbeta ya nne kati ya zile saba husababisha jua na mwezi kuwa giza (Ufunuo 8:12). Matokeo ya tarumbeta ya tano yatakuwa pigo la " kipepo la nzige" ambayo yatashambulia na kuwatesa wanadamu (Ufunuo 9:1- 11). Baragumu ya sita inatoa jeshi la mapepo ambayo itaua thuluthi moja ya binadamu (Ufunuo 9:12-21). Baragumu ya saba itaita malaika wa saba wenye mabakuli hayo saba ya ghadhabu ya Mungu (Ufunuo 11:15-19, 15:1-8).

Hukumu ya bakuli ya saba imeelezewa katika Ufunuo 16:1-21. Hukumu ya bakuli la saba iliyoitwa na baragumu ya saba. Bakuli ya kwanza husababisha vidonda vyenye maumivu yatakayo wakumba wanadamu (Ufunuo 16:2). Matokeo ya bakuli la pili ni kifo cha kila kilicho hai katika bahari (Ufunuo 16:3). Bakuli la tatu husababisha mito kubadilika na kuwa damu (Ufunuo 16:4-7). La nne kati ya yale mabakuli saba litasababisha joto la jua litakalozidi na kusababisha maumivu makubwa (Ufunuo 16:8-9). Bakuli la tano litasababisha giza kubwa na kuongezeka kwa vidonda vya bakuli la kwanza (Ufunuo 16:10-11). Matokeo ya bakuli la sita ni katika mto wa Frati kuwa kavu na majeshi ya Mpinga Kristo waliokuwa wamekusanyika pamoja kupigana vita ya Amagedoni (Ufunuo 16:12-14). Matokeo ya bakuli la saba ni tetemeko la ardhi na kufuatiwa na mvua ya theluji kubwa (Ufunuo 16:15-21).

Ufunuo 16:5-7 yamtangaza Mungu, "Wewe u mwenye haki, uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu, kwa kuwa umehukumu hivi, kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe, nao wamestahili. Nikaisikia hiyo madhabahu ikisema, Naam, Wbana Mungu Mwenyezi, na sa kweli na za haki, hukumu zako."

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Mihuri saba na tarumbeta saba katika kitabu cha Ufunuo ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries