settings icon
share icon
Swali

Majaliwa ya kipekee ni nini?

Jibu


Majaliwa ya kipekee ni njia Mungu na kupitia kwayo Mungu anasimamia vitu vyote katika ulimwengu. Mafundisho ya majaliwa yanadai kwamba Mungu ana udhibiti wote wa kila kitu. Hii ni pamoja na ulimwengu kwa ujumla (Zaburi 103:19), ulimwengu wa kimwili (Mathayo 5:45), mambo ya mataifa (Zaburi 66:7), uzao wa binadamu na hatima (Wagalatia 1:15), mafanikio ya binadamu na kushindwa (Luka 1:52), na ulinzi wa watu wake (Zaburi 4:8). Mafundisho haya yanapinga dhana kwamba ulimwengu unaongozwa na nafasi au hatima.

Kusudi, au lengo la majaliwa ya kipekee ni kukamilisha mapenzi ya Mungu. Kuhakikisha kuwa malengo yake yametimia, Mungu anasimamia mambo yote ya mwanadamu na kazi kwa njia ya asili ya mpangilio wa mambo. Sheria za asili sio kitu kingine zaidi kuliko picha ya Mungu katika kazi ulimwenguni. Sheria za asili hazina uwezo wa asili, wala kufanya kazi kwa kujitegemea. Sheria za asili ni kanuni na misingi Mungu anaweka katika nafasi ili kusimamia jinsi mambo yatakavyo kuwa.

Hiyo pia huwa kwa ajili ya uchaguzi wa binadamu. Kwa maana halisi sisi hatuko huru kuchagua au kutenda mbali na mapenzi ya Mungu. Kila kitu sisi hufanya na kila kitu sisi huchagua ni kwa mujibu kamili na mapenzi ya Mungu hata uchaguzi wetu wa dhambi (Mwanzo 50:20). Cha msingi kabisa ni kwamba Mungu hudhibiti uchaguzi na matendo yetu (Mwanzo 45:5; Kumbukumbu la torati 8:18, Mithali 21:1), lakini anafanya hivyo kwa namna ambayo haikiuki wajibu wetu kama mawakala huru wa maadili, wala kukanusha hali halisi ya uchaguzi wetu.

Mafundisho ya majaliwa ya kipekee yanaweza wekwa kwa muhtasari njia hii: "Mungu katika milele iliyopita, katika shauri la mapenzi yake, aliyeteua kila kitu kile ambacho kitatokea; lakini bila maana ni Mungu muumba wa dhambi; wala uwajibikaji wa binadamu haujaondolewa." njia ya msingi ambayo Mungu hutimiza mapenzi yake kwa njia ya sababu ya pili (kwa mfano, sheria za asili, uchaguzi binadamu). Kwa maneno mengine, Mungu hufanya kazi moja kwa moja kupitia sababu hizi sekondari ili kutimiza mapenzi yake.

Mungu pia wakati mwingine hufanya kazi moja kwa moja ili kutimiza mapenzi yake. Kazi hizi ni zile sisi huita miujiza (yaani, matukio ya kawaida kinyume na asili). Miujiza ni tekelezo la Mungu, kwa kipindi cha muda mfupi, ili asili ya vitu itimize mapenzi na kusudi lake. Mifano miwili kutoka kitabu cha Matendo inapaswa kutumikia kuonyesha Mungu anafanya kazi moja kwa moja na kutimiza mapenzi yake. Katika Matendo 9 tunaona uongofu wa Sauli wa Tarso. Kwa kufumba na kufumbua mwanga ukifuatwa na sauti ambayo Sauli / Paulo ni yeye pekee aliisikia, Mungu aliyabadilisha maisha yake milele. Ilikuwa ni mapenzi ya Mungu kumtumia Paulo zaidi kukamilisha mapenzi yake, na Mungu alitumia njia ya moja kwa moja kumbadili Paulo. Kuzungumza na mtu yeyote ambaye ameongofu kwa Ukristo, na hunenda kamwe usisikie hadithi kabisa kama hii. Wengi wetu huja kwa Kristo kwa kusikia mahubiri au kusoma kitabu au ushahidi wa mara kwa mara wa rafiki au familia. Fauka ya hayo, kuna kwa kawaida hali ya maisha ambayo huandaa njia -hasara ya kazi, kumpoteza mtu katika familia, ndoa ilyo vunjika, tawaliwa na madawa ya kulevya. Ubadilisho wa Paulo ulikuwa wa moja kwa moja na usio wa kawaida.

Katika Matendo 16:6-10, tunamwona Mungu akikamilisha mapenzi yake njia isiyo ya moja kwa moja. Hii inafanyika wakati wa safari ya pili ya Paulo ya umishenari. Mungu alimtaka Paulo na wenzake kwenda Troa, lakini wakati Paulo alipoondoka Antiokia ya Pisidia, alitaka kwenda mashariki katika Asia. Biblia inasema kwamba Roho Mtakatifu aliwakataza kunena neno katika Asia. Kisha walitaka kwenda magharibi katika Bithinia, lakini Roho wa Kristo hakuwaruhusu wao, kwa hivyo waliishia kwenda Troa. Hii iliandikwa katika hali ya ukumbusho, lakini wakati huo kulikuwa na pengine baadhi ya maelezo mantiki kwa nini hawakuweza kwenda katika maeneo hayo mawili. Hata hivyo, baada ya ukweli, waligundua kwamba ilikuwa ni Mungu awaelekeze kwenye Aliwataka waende- hii ni majaliwa ya kiungu. Mithali 16:9 yasema kuhusu hili: "moyo wa mtu haufikiri njia yake, bali Bwana huziongoza hatua zake."

Kwa upande mwingine, kuna wale ambao husema kwamba dhana ya Mungu moja kwa moja au kuchochea mambo yote huharibu uwezekano wowote wa mapenzi huru. Kama Mungu ako na udhibiti kamili, jinsi gani tunaweza kuwa huru kweli katika maamuzi tunayofanya? Kwa maneno mengine, ili hiari iwe na maana, lazima kuna baadhi ya mambo ambayo yako nje ya uhuru wa udhibiti wa Mungu -kwa mfano uendelevu wa kizazi cha binadamu. Hebu tutadhanie kwa ajili ya mjadala kwamba hii ni kweli. Ni nini basi? Kama Mungu hana udhibiti kamili wa dharura zote, basi, ni jinsi angeweza kuhakikisha wokovu wetu? Paulo anasema katika Wafilipi 1: 6 kwamba "Nami niliminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku y aKristo Yesu." Kama Mungu hana udhibiti wa mambo yote, basi ahadi hii, na ahadi zengine zote za Biblia ni batili. Tunaweza kuwa na usalama kamili kwamba kazi njema ya wokovu ilikuwa imeanzishwa ndani yetu itapelekwa hadi ukamilisho.

Aidha, kama Mungu hana udhibiti wa mambo yote, basi hakika Yeye si mweza yote, na kama si mweza yote, kisha yeye si Mungu. Kwa hiyo, bei ya kudumisha uendelevu nje ya udhibiti wa Mungu matokeo yake ni kuwa na Mungu ambaye siMungu kamwe. Na kama "uhuru" wetu unaweza zidi majaliwa, kisha hatimaye ni nani Mungu? Ni sis. Hii iko wazi, haikubaliki na mtu yeyote kwa mtazamo wa dunia Mkristo na Biblia. Majaliwa haiaribu uhuru wetu. Badala yake, majaliwa ndio kitu kinatuwezesha kutumia vizuri uhuru huo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Majaliwa ya kipekee ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries