settings icon
share icon
Swali

Je! Inamaanisha nini kuuacha mwili?

Jibu


Kifungu “kuuacha mwili” kinapatikana katika 2 Wakorintho 5:6-8. Paulo anasema kwamba ana uhakika katika hatima yake ya milele na anatamani siku ambayo anaweza “kuuacha mwili huu” na kwenda kukaa pamoja na Bwana anayempenda na kumtumikia. Mtu “kuuacha mwili wake inamaanisha kufa, kwa sababu wakati wa kifo, roho hutenganishwa na mwili na kuingia katika makao yake ya milele-mbinguni pamoja na Bwana au kuzimu, ukiwa umetengwa na Mungu milele.

Vivyo hivyo, Wakristo daima wana ujasiri, wakijua kwamba wakati tuko nyumbani katika mwili sisi huwa mbali na Mungu. Kwa maana tunatembea kwa imani, si kwa kuona. Tuna ujasiri, naam, tunafurahi zaidi kwa kuuacha mwili na kuwa pamoja na Bwana. Muumini aliyezaliwa mara ya pili anapokufa, nafsi yake huenda mara moja katika uwepo wa Bwana. Huku roho ikingojea kwa uangalifu ufufuo wa mwili. Paulo aliandikia kanisa la Filipi kutoka katika gereza la Kirumi:

Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida. Kama nitaendelea kuishi katika mwili, kwangu hili ni kwa ajili ya matunda ya kazi. Lakini sijui nichague lipi? Mimi sijui! Ninavutwa kati ya mambo mawili: Ninatamani kuondoka nikakae pamoja na Kristo, jambo hilo ni bora zaidi. 24Lakini kwa sababu yenu ni muhimu zaidi mimi nikiendelea kuishi katika mwili” (Wafilipi 1:21-24).

Shauku ya Paulo katika maisha ilikuwa kumtukuza Bwana Yesu Kristo. Ikiwa angeishi, angeelendea kufanya kazi kwa ajili ya Bwana. Ikiwa angekabiliwa na kuuawa, angeondoka katika maisha haya na kuwa pamoja na Kristo. Alikuwa na hamu ya kuwa pamoja na Mwokozi wake, lakini kama angebaki duniani, angeweza kuendelea kuwahudumia wengine.

Wapo wanaoamini kulala kwa nafsi, ikimaanisha kwamba mtu anapokufa, mwili na roho yake hulala kaburini, vikingoja ufufuo. Lakini kama hii ingekuwa kweli, kwa nini Paulo hangependa kuishi ili kuhudumu kwa muda mrefu iwezekanavyo, badala ya kulala kaburini? Na kama ingekuwa kweli kwamba mwili na roho havitenganishwi kamwe, isingewezekana kabisa kutokuwepo kwenye mwili na kuwepo pamoja na Bwana.

Tunahitimisha, basi, kwamba waumini wanaokufa kwa hakika hawapo katika miili yao bali wako pamoja na Bwana katika furaha fahamu wakingojea siku hiyo kuu ya ufufuo!

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Inamaanisha nini kuuacha mwili?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries