settings icon
share icon
Swali

Ni kwa nani tunapaswakuomba kwa Baba, kwa Mwana, au kwa Roho Mtakatifu?

Jibu


Maombi yote lazima yaelekezwe kwa utatu wa Mungu wetu -Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Biblia inafundisha kwamba tunaweza kuomba kwa mmoja au wote watatu, kwa sababu wote watatu ni moja. Pamoja na mtunzi zaburi tunaomba kwa Baba, "Uisikie sauti ya kilio changu, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu kwa maana wewe ndiwe nikuombaye. " ( Zaburi 5:2). Tunaomba kwa Bwana Yesu, kama vile kwa Baba kwa sababu wao ni sawa. Maombi kwa mwanachama mmoja wa utatu ni sala kwa wote. Stefano, alipokuwa akiuawa, aliomba "Bwana Yesu, pokea roho yangu " (Matendo 7:59). Sisi pia tunapaswa kuomba katika jina la Kristo. Paulo aliwahimiza waumini wa Efeso daima kutoa "shukrani kwa Mungu Baba kwa kila kitu, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo" (Waefeso 5:20 ). Yesu aliwahakikishia wanafunzi wake kwamba wakiulizwa katika jina lake- maana katika mapenzi yake watapewa (Yohana 15:16; 16:23). Vile vile, tunaambiwa kumwomba Roho Mtakatifu na katika nguvu zake. Roho anatusaidia kuomba, hata wakati hatujui nini au namna gani kuomba (Warumi 8:26; Yuda 20). Labda njia nzuri kuelewa jukumu la utatu katika maombi ni kwamba tunaomba kwa Baba, kwa njia ya (au katika jina la ) Mwana, kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Wote watatu ni washirika hai katika sala ya waumini.

Muhimu vile vile ni kwa yule hatupaswi kuomba. Baadhi ya dini zisizo za kikristo uhamasisha wafuasi wao kuomba kwa miungu yote ya dini, jamaa waliokufa, watakatifu wa Mungu, na roho. Wakatoliki wa Kirumi hufundishwa kumwomba Maria na watakatifu mbalimbali. Sala hizo sio za kimaandiko na hakika ni chukizo kwa Baba yetu wa mbinguni. Kuelewa ni kwa nini, tunahitaji tu kuangalia asili ya maombi. Maombi yana mambo kadhaa, na kama sisi tutaangalia baadhi ya mawili - sifa na shukrani - tunaweza kuona kwamba maombi ni, ibada kuwa katika msingi wake. Tunapomsifu Mungu, sisi humuabudu kwa sifa zake na kazi yake katika maisha yetu. Wakati tunatoa maombi ya shukrani, sisi huabudu wema wake, huruma na fadhili kwetu. Ibada inatoa utukufu kwa Mungu mmoja ambaye anastahili utukufu. Tatizo la kuomba kwa mtu yeyote zaidi ya Mungu ni kwamba Yeye hashiriki utukufu wake. Kwa kweli, kuomba kwa mtu yeyote au kitu kingine chochote zaidi ya Mungu ni ibada ya sanamu. "Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa wmingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu" (Isaya 42:8).

Mambo mengine ya sala kama vile toba, kukiri, na dua pia ni aina ya ibada. Sisi hutubu tukijua kwamba Mungu, ni Mungu mwenye kusamehe na upendo na Yeye imetoa njia ya msamaha katika sadaka ya mwana wake juu ya msalaba. Tukiziungama dhambi zetu kwa sababu Yeye anasijua "Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote" ( 1 Yohana 1:9) na sisi humwabudu kwa ajili ya hiyo. Sisi huja kwake kwa maombi yetu na maombezi kwa sababu tunajua anatupenda na kutusikiliza, na sisi humwabudu kwa huruma na wema wake kwa kuwa tayari kutusikia na kutujibu. Wakati tunaona yote haya, ni rahisi kuona kwamba kuomba kwa mtu mwingine zaidi ya utatu ni jambo lisilo fikirika kwa sababu sala ni aina ya ibada, na ibada ni akiba ya ajili Mungu peke yake. Sisi huomba kwa nani? Jibu ni Mungu. Kuomba kwa Mungu peke yake, ni muhimu zaidi kuliko Mtu wa Utatu sisi huwasilisha maombi yetu kwake.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kuomba kwa Baba, kuomba kwa Mwana, kuomba kwa Roho ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries